CAF Kufanya Droo ya Kufuzu AFCON 2027 Leo Jumanne Mei 19, 2026

CAF Kufanya Droo ya Kufuzu AFCON 2027 Leo Jumanne Mei 19, 2026

CAF itafanya droo ya kufuzu fainali za TotalEnergies CAF Africa Cup of Nations 2027 leo Jumanne, Mei 19, 2026, katika makao makuu ya Shirikisho la Soka la Misri mjini Cairo.

Droo hiyo itaanza saa 9:00 alasiri kwa saa za Afrika Mashariki na itapanga njia ya timu zitakazowania nafasi ya kushiriki michuano ya AFCON 2027, ambayo itaandaliwa kwa pamoja na Kenya, Tanzania na Uganda.

KipengeleMaelezo
TukioDroo ya kufuzu AFCON 2027
TareheJumanne, Mei 19, 2026
MudaSaa 9:00 alasiri kwa saa za Afrika Mashariki
MahaliMakao makuu ya EFA, Cairo, Misri
Timu shiriki48
Makundi12 ya timu nne nne
Timu zitakazofuzu24
WaandaajiKenya, Tanzania na Uganda
Fainali za AFCON 2027Juni 19 hadi Julai 17, 2027

CAF Kufanya Droo ya Kufuzu AFCON 2027 Leo Jumanne Mei 19, 2026

Jumla ya timu 48, zikiwemo nchi tatu wenyeji Kenya, Tanzania na Uganda, zitashiriki hatua ya kufuzu. Timu hizo zitapangwa katika makundi 12, kila kundi likiwa na timu nne.

Kwa mfumo uliowekwa, timu mbili za juu katika kila kundi zitafuzu kwa fainali. Katika makundi yatakayokuwa na moja ya nchi wenyeji, timu moja ya ziada itaendelea.

Ratiba ya mechi za kufuzu imepangwa kuchezwa katika madirisha matatu ya kalenda ya kimataifa ya FIFA kabla ya fainali za mwaka 2027. Mechi za kwanza na za pili zitachezwa kati ya Septemba 21 na Oktoba 6, 2026. Mechi za tatu na nne zitafanyika kati ya Novemba 9 na 17, 2026, huku mechi za tano na sita zikipangwa kuchezwa Machi 22 hadi 30, 2027.

Fainali za AFCON 2027 zitaanza Juni 19, 2027, huku mchezo wa fainali ukipangwa kuchezwa Julai 17, 2027.

Droo Kurushwa Moja kwa Moja

Mashabiki wataweza kufuatilia matukio yote yatakayokua yanaendelea wakati droo  ikifanyika mubashara na moja kwa moja kupitia SuperSport, BeIN Sport, Canal+, Azam TV, New World TV, SABC Sport, ERTU, KBC, TBC Tanzania.

CAF TV kupitia YouTube pia itarusha droo hiyo moja kwa moja, huku maudhui ya nyuma ya pazia yakitarajiwa kupatikana kupitia majukwaa ya kidijitali ya CAF.

Droo hiyo itaendeshwa na magwiji wa soka la Afrika Max-Alain Gradel wa Cote d’Ivoire, William Troost-Ekong wa Nigeria, Essam El Hadary wa Misri na Trésor Mputu wa DR Congo.

Umuhimu wa Droo kwa AFCON 2027

Droo ya leo ni hatua muhimu katika maandalizi ya AFCON 2027 kwa sababu itaonyesha njia ya kila timu kuelekea fainali. Kwa mashabiki wa Tanzania na Afrika Mashariki, michuano hiyo ina mvuto mkubwa zaidi kwa kuwa Tanzania ni mmoja wa waandaaji wenza pamoja na Kenya na Uganda.

Mashindano hayo pia yatarejesha fainali za AFCON Afrika Mashariki kwa mara ya kwanza baada ya miaka 51, jambo linaloongeza uzito wa toleo la 2027.

Kwa ujumla, droo ya kufuzu AFCON 2027 itatoa picha rasmi ya safari ya timu 48 zitakazowania nafasi 24 za kushiriki fainali. Macho ya mashabiki sasa yataelekezwa Cairo, ambako makundi ya kufuzu yatapangwa leo alasiri.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Ratiba ya Nusu Fainali CRDB Federation Cup 2026
  2. Fiston Mayele atajwa kikosi cha DR Congo Kombe la Dunia 2026
  3. Chama Aendelea Kung’ara Simba Ikifuzu Nusu Fainali CRDB Federation Cup
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo