Mfungaji Bora Ligi Kuu ya NBC 2025/2026

Mfungaji Bora Ligi Kuu ya NBC 2025/2026 ni Mossi Ndumumwe

Mfungaji Bora Ligi Kuu ya NBC 2025/2026 ni mshambuliaji wa Singida Black Stars, Mossi Ndumumwe, aliyemaliza msimu akiwa na mabao 17 na kuongoza orodha ya wafungaji wa ligi.

Mfungaji Bora Ligi Kuu ya NBC 2025/2026

Ndumumwe amewazidi wapinzani wake wa karibu baada ya kumaliza juu ya jedwali la wafungaji, huku Feisal Salum wa Azam akifuata nafasi ya pili akiwa na mabao 15. Kiungo wa Young Africans, Allan Okello, ameshika nafasi ya tatu kwa kufunga mabao 14.

Wafungaji Bora wa Ligi Kuu ya NBC 2025/2026

Jedwali la wafungaji bora wa NBC Premier League msimu wa 2025/2026 limekamilika kama ifuatavyo:

Nafasi

MchezajiKlabuMagoli
1Mossi NdumumweSingida BS17
2Feisal SalumAzam15
3Allan OkelloYoung Africans14
4Mathew TegisiPamba Jiji11
5Fabrice Wa NgoyNamungo11
6Pacome ZouzouaYoung Africans9
7Mudathir YahyaYoung Africans9
8Prince DubeYoung Africans9
9Selemani MwalimuSimba9
10Paul PeterJKT Tanzania9
11Maabad MaulidCoastal Union8
12Iddy SelemaniAzam8
13Clatous ChamaSimba8
14Saleh KarabakaJKT Tanzania8
15Laurindo Dilson DepuYoung Africans8
16William EdgarDodoma Jiji7
17George MpoleTanzania Prisons7
18Libasse GueyeSimba7
19Jephte KitambalaAzam7
20Elie MpanzuSimba7
21Chukwunonye ObasiFountain Gate6

Ndumumwe Aongoza Mbio za Ufungaji

Mossi Ndumumwe ameumaliza msimu akiwa kinara wa mabao kwa kufunga mara 17 na hivyo kutwaa heshima ya kuwa Mfungaji Bora Ligi Kuu ya NBC 2025/2026. Nyuma yake anafuatia Feisal Salum wa Azam mwenye mabao 15, huku Allan Okello wa Young Africans akimaliza nafasi ya tatu kwa mabao 14.

Young Africans Yatoa Wachezaji Wengi Kwenye Orodha

Young Africans ndiyo klabu yenye wachezaji wengi zaidi ndani ya orodha ya wafungaji bora wa msimu huu. Mbali na Allan Okello aliyemaliza na mabao 14, klabu hiyo pia ina Pacome Zouzoua, Mudathir Yahya na Prince Dube waliomaliza na mabao tisa kila mmoja pamoja na Laurindo Dilson Depu aliyefunga mabao nane.

Simba, Azam na Klabu Nyingine Pia Zawakilishwa

Simba imeingiza Selemani Mwalimu, Clatous Chama, Libasse Gueye na Elie Mpanzu kwenye mbio za kuwania kiatu cha dhahabu ambapio nyota hao wote wameshindwa kufikia idaki ya magoli ya Mossi. Azam imewakilishwa na Feisal Salum, Iddy Selemani na Jephte Kitambala, huku JKT Tanzania ikiwa na Paul Peter na Saleh Karabaka.

Pamba Jiji, Namungo, Coastal Union, Dodoma Jiji, Tanzania Prisons na Fountain Gate pia zimekuwa na wachezaji walioingia kwenye orodha ya wafungaji bora wa NBC Premier League msimu wa 2025/2026.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Kikosi cha Yanga vs JKT Tanzania Leo 30/06/2026
  2. JKT Tanzania vs Yanga Leo 30/06/2026 Saa Ngapi?
  3. Ratiba ya Ligi Kuu NBC Leo Juni 30, 2026: Yanga, Simba Kuamua Ubingwa Raundi ya Mwisho
  4. Simba Yatoa Tamko Kuhusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Kuchezwa Pemba
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo