Ratiba ya Ligi Kuu Ya NBC Leo May 2 2026
Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/2026 inaendelea leo Jumamosi, Mei 2, 2026, huku mashabiki wa soka nchini wakitarajia kushuhudia michezo miwili muhimu itakayochezwa katika viwanja tofauti. Ratiba ya leo inahusisha timu nne ambazo zote zinahitaji matokeo chanya katika hatua hii ya msimu.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa, michezo yote ya leo itarushwa moja kwa moja kupitia AzamSports1HD, ikitoa fursa kwa mashabiki kufuatilia kwa karibu matukio yote ya viwanjani.
Ratiba ya Michezo ya Ligi Kuu Ya NBC Leo
Katika mchezo wa kwanza wa siku, Mtibwa Sugar watakuwa nyumbani katika dimba la KMC Complex kuikaribisha Azam FC. Mchezo huu unatarajiwa kuanza majira ya saa 10:00 jioni.
Baadaye usiku, kutakuwa na pambano lingine ambapo Coastal Union watakuwa katika uwanja wa Mkwakwani, Tanga, wakiwakaribisha Singida BS. Mechi hii imepangwa kuanza saa 12:30 jioni.
Muhtasari wa Michezo ya Leo
Mtibwa Sugar vs Azam FC
- Saa 10:00 jioni
- Uwanja: KMC Complex
Coastal Union vs Singida BS
- Saa 12:30 jioni
- Uwanja: Mkwakwani, Tanga
Mapendekezo ya Mhariri:









Leave a Reply