Orodha ya Majina ya Samia Scholarship 2026/2027

Orodha ya Majina ya Samia Scholarship 2026/2027

Orodha ya majina ya wanafunzi wanaoruhusiwa kuomba Samia Scholarship 2026/2027 imetolewa, ikijumuisha wanafunzi 1,000 waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita wa mwaka 2026.

Wanafunzi waliopo kwenye orodha hiyo wametoka katika tahasusi za sayansi na wanaruhusiwa kuwasilisha maombi yao kwa njia ya mtandao kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB).

Maombi ya Samia Scholarship 2026/2027 yanafanyika kuanzia Julai 28 hadi Agosti 31, 2026. Orodha rasmi ina majina ya wanafunzi 1,000 pamoja na namba zao za mtihani.

Muhimu: Kuonekana kwa jina kwenye orodha hakumaanishi mwanafunzi tayari amepewa ufadhili. Orodha hiyo inawataja wanafunzi wanaoruhusiwa kuomba. Mwombaji anatakiwa kukamilisha maombi na kutimiza vigezo vilivyowekwa.

Orodha ya Majina ya Samia Scholarship 2026/2027

Nani Anaruhusiwa Kuomba Samia Scholarship 2026/2027?

Kwa mujibu wa mwongozo wa HESLB, mwombaji anatakiwa kuwa Mtanzania na awe na ufaulu wa juu katika ACSEE 2026 kwenye mojawapo ya tahasusi zifuatazo:

  1. PCM: Fizikia, Kemia na Hisabati
  2. PCB: Fizikia, Kemia na Baiolojia
  3. PGM: Fizikia, Jiografia na Hisabati
  4. CBG: Kemia, Baiolojia na Jiografia
  5. PMC: Fizikia, Hisabati na Kompyuta
  6. CBA: Kemia, Baiolojia na Kilimo
  7. CBN: Kemia, Baiolojia na Lishe

Mwombaji pia anatakiwa kuwa miongoni mwa wanafunzi waliotajwa kwenye orodha iliyochapishwa kwa ajili ya maombi ya Samia Scholarship.

Aidha, anatakiwa kupata udahili katika taasisi ya elimu ya juu inayotambuliwa ili kusoma programu inayohusiana na Sayansi Asilia, Teknolojia, Uhandisi, Hisabati au Sayansi za Afya katika mwaka wa masomo 2026/2027.

Maombi yanapaswa kujazwa kwa usahihi kupitia mfumo wa OLAMS. Mwombaji pia hatakiwi kuwa mnufaika wa ufadhili mwingine, isipokuwa pale ufadhili huo unapogharamia sehemu ya gharama ambazo hazijafadhiliwa na HESLB.

Mahitaji Muhimu Wakati wa Kuomba

Wanafunzi waliopo kwenye orodha wanapaswa kusoma na kufuata taratibu zote za maombi. Mwongozo unamtaka mwombaji kuwa na:

  1. Anwani ya makazi ya kidijitali ya NaPA.
  2. Namba ya NIDA kwa mwombaji mwenye umri wa miaka 18 au zaidi.
  3. Cheti cha kuzaliwa kilichohakikiwa na RITA au ZCSRA.
  4. Akaunti ya benki iliyo hai na yenye jina linalofanana na lililopo kwenye cheti cha CSEE.
  5. Namba ya simu iliyosajiliwa na inayopatikana.

Waombaji waliozaliwa nje ya Tanzania wanatakiwa kupata barua kutoka RITA au ZCSRA inayothibitisha taarifa zao za kuzaliwa.

Kabla ya kuwasilisha maombi, mwanafunzi anatakiwa kukagua taarifa zote, kurekebisha makosa na kuhakikisha fomu imejazwa na kusainiwa. Udanganyifu au kughushi nyaraka kunaweza kusababisha mwombaji kuondolewa katika mchakato wa maombi na kuchukuliwa hatua nyingine za kisheria.

Samia Scholarship Inagharamia Nini?

Wanafunzi watakaofanikiwa kupata Samia Scholarship watapangiwa viwango vya ufadhili kulingana na mahitaji ya programu wanazosoma.

KipengeleKiasi kinachotolewa
Ada ya masomoHadi TZS 5,000,000 kwa mwaka
Chakula na malaziTZS 10,000 kwa siku
Vitabu na vifaa vya kuandikiaHadi TZS 200,000 kwa mwaka
Mafunzo kwa vitendoTZS 10,000 kwa siku, hadi siku 56
Gharama za utafitiHadi TZS 500,000 kwa mwaka
Bima ya afyaTZS 50,400 kwa mwaka
Vifaa saidizi kwa mwanafunzi mwenye mahitaji maalumuHadi TZS 2,000,000 mara moja

Ufadhili pia unaweza kugharamia mahitaji maalumu ya kitivo kwa programu zinazohitaji vifaa au mahitaji ya ziada. Kiasi hicho kitatolewa kwa kuzingatia viwango vilivyowekwa na HESLB.

Muda na Mfumo wa Malipo

Mwanafunzi atakayepata Samia Scholarship anaweza kufadhiliwa kwa kipindi cha miaka mitatu hadi mitano, kulingana na muda wa programu anayosomea.

Malipo yatafanyika kupitia mfumo wa HESLB Digital Disbursement Solution, unaofahamika kama DiDiS. Ada ya masomo italipwa moja kwa moja kwenye akaunti ya benki ya taasisi husika, huku fedha za vipengele vingine zikilipwa kwenye akaunti ya mwanafunzi.

Fedha za chakula na malazi zitatolewa kwa awamu nne kwa mwaka.

Masharti ya Kuendelea na Samia Scholarship

Mnufaika anatakiwa kusoma na kuelewa mwongozo pamoja na kusaini makubaliano ya ufadhili na HESLB.

Ufadhili unaweza kusitishwa ikiwa mwanafunzi:

  • Ataahirisha masomo kwa sababu zisizohusiana na matibabu.
  • Atafukuzwa chuoni kutokana na sababu za kitaaluma au kinidhamu.
  • Atapata GPA iliyo chini ya 3.8 katika mwaka wa masomo.

Mwanafunzi anayeahirisha masomo kwa sababu za kiafya anaweza kuendelea na ufadhili endapo sababu hiyo itathibitishwa kwa maandishi na taasisi anayosomea.

Wanafunzi watakaofanikiwa kupata ufadhili watajulishwa kuhusu mgao wao kupitia akaunti zao za SIPA.

Jinsi ya Kuangalia Orodha ya Majina ya Samia Scholarship 2026/2027

Orodha rasmi ina majina ya wanafunzi 1,000 pamoja na namba zao za mtihani. Mwanafunzi anatakiwa kuangalia jina au namba yake ya mtihani kwa umakini kabla ya kuanza maombi.

Bofya hapa kuangalia au kupakua orodha kamili ya majina ya Samia Scholarship 2026/2027.

Wanafunzi waliopo kwenye orodha wanapaswa kukamilisha maombi yao kupitia HESLB kabla ya Agosti 31, 2026, kuhakikisha taarifa na nyaraka zote zilizowasilishwa ni sahihi.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Matokeo ya Kidato cha Sita 2026: Haya Hapa ACSEE Results
  2. Matokeo ya Kidato cha Sita 2026 NECTA Form Six Results
  3. Dirisha la Maombi ya Vyuo 2026/2027 Lafunguliwa, TCU Yataja Tarehe ya Mwisho
  4. NECTA Yatangaza Matokeo ya Kidato cha Sita 2026/2027
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo