Zahera Afurahishwa na Ushindi Namungo, Awataka Wachezaji Kuongeza Bidii

Zahera Afurahishwa na Ushindi Namungo, Awataka Wachezaji Kuongeza Bidii

Baada ya Namungo kupata ushindi wa bao 1-0 juzi tarehe 28 dhidi ya Tanzania Prisons, kocha mkuu wa timu hiyo Mkongomani, Mwinyi Zahera amesema, ameridhika na viwango vya wachezaji walivyovionyesha huku akiwataka kuendelea kupambana zaidi ya hapo.

Zahera aliyekalia kuti kavu la kutimuliwa kikosini humo, amezungumza hayo baada ya timu hiyo kupata ushindi huo ukiwa ni wa pili mfululizo kufuatia kuifunga Coastal Union mabao 2-0, mechi ikipigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Septemba 17.

“Kadri unavyozidi kupoteza mchezo ndivyo ambavyo hata morali ya wachezaji kiujumla inashuka lakini nashukuru mechi hizi mbili zimekuwa na utofauti mkubwa kwa sababu wachezaji wametimiza majukumu yao vizuri, yaliyotupatia matokeo chanya.”

Zahera Afurahishwa na Ushindi Namungo, Awataka Wachezaji Kuongeza Bidii

Kocha huyo aliyejiunga na Namungo Desemba 30, 2023 akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Denis Kitambi alisema, moja ya changamoto kubwa iliyopo ndani ya kikosi hicho ni kutokuwa na balansi nzuri katika safu ya uzuiaji na ushambuliaji.

“Michezo miwili ya mwisho ndio tumekuwa na balansi nzuri lakini ukiangalia tangu tumeanza Ligi tumekuwa tukiruhusu bao, sio mwenendo mzuri kwetu ingawa jambo kubwa ni kupata matokeo chanya ili kupunguza presha ambayo ilianza kujitokeza.”

Namungo ilianza Ligi Kuu msimu huu kwa kupoteza michezo mitatu ikichapwa 2-1 na Tabora United, 2-0 dhidi ya Fountain Gate na 1-0 kutoka kwa Dodoma Jiji kisha kuzinduka kuanzia kwa Coastal Union na Prisons.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Gamondi na Davids waleta ladha ya Ulaya Ndani ya Soka la Bongo
  2. Azam Yashindwa Kutamba Ugenini, Singida yarejea kileleni
  3. Manchester United Yapigwa Tena Nyumbani, Hali Yazidi Kuwa Ngumu Old Trafford
  4. Ahoua Aipa Simba Pointi Tatu Muhimu Uwanja wa Jamhuri
  5. Matokeo ya Yanga Vs KMC Leo 29 September 2024
  6. Matokeo ya Simba Sc vs Dodoma Jiji Leo 29/09/2024
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo