Matokeo ya Simba Sc vs Dodoma Jiji Leo 29/09/2024

Matokeo ya Simba Sc vs Dodoma Jiji Leo 29/09/2024 | Matokeo ya Simba Leo Dhidi ya Dodoma Jiji | Matokeo ya Dodoma Jiji Vs Simba Sc Leo Live Ligi Kuu Tanzania Bara

Wekundu wa Msimbazi Simba SC leo wanashuka dimbani kuikabili Dodoma Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania majira ya saa 12:30 jioni katika Uwanja wa Jamhuri Stadium, jijini Dodoma. Mchezo huu unatarajiwa kuwa wa kusisimua kutokana na hali ya timu zote mbili katika msimu huu wa ligi, huku Simba wakiwa na rekodi nzuri ya ushindi wa mechi tatu mfululizo tangu kuanza kwa msimu huu.

Simba SC imeanza msimu huu ikionesha uwezo wa hali ya juu, ambapo hadi hivi sasa wameweza kushinda mechi zake zote tatu za awali na kufunga mabao 9 bila kuruhusu bao lolote. Hali hii inawapa nguvu zaidi kuelekea mchezo wa leo, huku wakitafuta kuongeza ushindi wa nne mfululizo. Kwa upande wa Dodoma Jiji, wamekuwa na mwanzo wa taratibu msimu huu, wakicheza mechi tano na kupata ushindi mara moja tu dhidi ya Namungo kwa bao 1-0. Timu hii pia imepata sare tatu na kufungwa mara moja na Mashujaa.

Rekodi za mechi zilizopita zinaonesha kwamba Dodoma Jiji hawajawahi kuibuka na ushindi wala sare dhidi ya Simba SC, kwani wamepoteza mechi zote nane walizokutana kwenye Ligi Kuu. Hali hii inatoa changamoto kubwa kwa Dodoma Jiji leo huku Simba SC wakitarajia kuendeleza rekodi yao bora dhidi ya wenyeji hao.

Kwa Simba SC, mshambuliaji Leonel Ateba anaonekana kuwa kwenye fomu nzuri baada ya kufunga mabao mawili katika mechi mbili zilizopita za mashindano tofauti. Mchezaji mwingine muhimu kwa Simba leo ni kiungo mshambuliaji Deborah Fernandez, ambaye ameonyesha ubora wake wa kuongoza safu ya ushambuliaji na kutoa pasi za mwisho zenye ubunifu mkubwa.

Kwa upande wa wapinzani wa Simba Sc leo, Dodoma Jiji, Paul Peter ni mshambuliaji wa kutegemewa na anaongoza orodha ya wafungaji wa timu hiyo msimu huu akiwa amefunga mabao mawili. Peter ana nafasi kubwa ya kujaribu kuvunja safu ya ulinzi ya Simba ambayo imekuwa ngumu kufungika katika michezo kadhaa iliopita. Pia, kiungo mshambuliaji Ibrahim Ajibu anatarajiwa kutoa mchango mkubwa katika eneo la kati la uwanja kwa upande wa Dodoma Jiji, akijaribu kupunguza nguvu ya Simba.

Matokeo ya Simba Sc vs Dodoma Jiji Leo 29/09/2024

Matokeo ya Simba Sc vs Dodoma Jiji Leo 29/09/2024

Dodoma Jiji 0-1 FT Simba Sc
  • Mchezo Umeanza; Dodoma Jiji 0-0 Simba Sc
  • Dakika ya 17; Dodoma Jiji 0-0 Simba Sports Club
  • Dakika ya 36; Dodoma Jiji 0-0 Simba Sports Club
  • Zimeongezwa Dakika 2 kabla ya kipindi cha kwanza kukamilika
  • Kipindi cha kwanza kimeisha, Dodoma Jiji 0-0 Simba Sc
  • Kipindi cha Pili Kimeanza, Dakika ya 46 Dodoma Jiji 0-0 Simba Sc
  • Simba wanapata Penati dakika ya 59 baada ya Mhuammed hussein kuchezewa rafu ndani ya box
  • Dakika ya 62, Simba inapata Goli la Kuongoza Baada ya Jean Charles Ahoua Kufunga Mkwaju wa penati
  • Dakika ya 76, Dodoma Jiji 0-1 Simba Sc
  • Dakika ya 87, Dodoma jiji 0-1 Simba SC | Debora Fernandez ametangazwa kama mchezaji bora wa mchezo
  • Dakika ya 90, Dodoma jiji 0-1 Simba SC

Picha Za Matukio Kutoka Uwanjani Mechi ya Dodoma Jiji vs Simba leo

Jaribio la kibu deni katika mchezo wa dodoma jiji vs Simba Wachezaji wa simba wanashambulia kwa kasi dhihi ya dodoma jiji

🏆 #NBCPremierLeague
⚽️ Dodoma Jiji Fc🆚Simba Sc
📆 29.09.2024
🏟 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma
🕖 18:30 (EAT)

Kauli za Wachezaji Kuelekea Mchezo Huu

Straika wa Dodoma Jiji, Waziri Junior, amesema kuwa wamejiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo huu na wanaingia dimbani kwa kujiamini. Alieleza kuwa kocha amewapa mbinu sahihi za kuwakabili Simba, na anaamini timu yao inaweza kupata matokeo mazuri, licha ya changamoto wanazokutana nazo. Waziri alisema: “Kocha ametuambia tuingie kwa kujiamini na kutumia nafasi zote tutakazopata, si rahisi kwa Simba kutoboa kwetu.”

Aidha, Ibrahim Ajibu ameongeza kuwa, mechi dhidi ya Simba haina utofauti mkubwa na mechi zingine walizocheza, ila wakiingia kwa heshima wakitambua ukubwa wa wapinzani wao. “Simba ni timu yenye mashabiki wengi, lakini tumejiandaa kuhimili presha hiyo na kufanya vizuri katika mchezo huu,” alisema Ajibu.

Mtazamo wa Kikosi cha Simba

Simba SC inakuja kwenye mchezo huu na matumaini makubwa ya kuendelea kuonyesha uwezo wao bora katika ligi. Kocha Robertinho anatarajiwa kuwategemea wachezaji wake nyota kama John Bocco, Clatous Chama, na Shomari Kapombe ili kuhakikisha wanapata ushindi muhimu wa kuweka nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi. Kwa Simba, mchezo huu ni fursa ya kuendelea kuweka rekodi nzuri na kuonyesha kuwa wanadhamira ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu kwa mara nyingine.

Kwa upande wa ulinzi, safu ya Simba inatarajiwa kuwa makini chini ya uongozi wa Henock Inonga na Mohamed Hussein, ambao wamekuwa wakiiongoza vyema safu ya ulinzi bila kuruhusu bao lolote katika mechi zilizopita.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Mashujaa vs Azam Leo 29/09/2024 Saa Ngapi?
  2. Yanga Vs KMC Leo 29/09/2024 Saa Ngapi?
  3. Ratiba ya Mechi za Ligi Kuu ya NBC Leo Septemba 29, 2024
  4. Dodoma Jiji Vs Simba Sc Leo 29/09/2024 Saa Ngapi
  5. Gomez Aanza Mikwara Ligi Kuu Bara, Aahidi Mabao Zaidi
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo