Matokeo Yanga VS Azam Leo Fainali Ngao ya Jamii 2024

Matokeo Yanga VS Azam Leo Fainali Ngao ya Jamii 2024 | Matokeo ya Yanga Vs Azam Leo 11/08/2024

Leo ndio leo, Fainali ya michuano ya Ngao ya jamii 2024 imewadia na mabingwa wa ligi kuu Tanzania Yanga sc watapambana vikali na wana rambaramba Azam Fc katika uwanja wa benjamin mkapa katika mtanange wa kumtafuta bingwa wa michuano ya Ngao ya jamii. Mechio hii itaanza saa moja usiku na inategemewa kuwa yenye ushindani mkali na soka la kuvutia.

Mtanange huu wa Ngao ya Jamii sio tu pambano la kawaida, bali ni mchezo wenye historia na hisia kali. Ni zaidi ya mechi ya ufunguzi wa msimu; ni mechi ya kisasi, ubabe, na utemi katika ulimwengu wa soka nchini Tanzania.

Yanga na Azam zimekutana mara nne kwenye Ngao ya Jamii, Yanga ikishinda mara tatu, na Azam mara moja tu – kwa penalti miaka minane iliyopita. Azam itaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wao wa mwisho dhidi ya Yanga katika fainali ya Kombe la Shirikisho, na watataka kulipa kisasi cha kupoteza kwa penalti katika Ngao ya Jamii mwaka 2016.

Yanga, kwa upande wao, watataka kuendeleza ubabe wao dhidi ya Azam na pia kulipa kisasi cha kupoteza mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Azam kwa mabao 2-1. Majeraha ya wachezaji muhimu kama Yao Kouassi na Pacome Zouzoua, yaliyotokana na mchezo huo, yaliathiri ushiriki wao katika Ligi ya Mabingwa Afrika, na Yanga haitasahau hilo kirahisi.

Pambano hili litakuwa pia ni vita ya mastaa wa soka Tanzania. Mashabiki watashuhudia upinzani mkali kati ya Aziz KI na Fei Toto, James Akaminko dhidi ya Khalid Aucho, na wengine wengi. Makipa Diarra Djigui wa Yanga na Mohamed Mustafa wa Azam watakuwa na kazi kubwa ya kuzuia michomo ya washambuliaji hatari kama Aziz KI, Clement Mzize, Gjibril Sillah, na Fei Toto.

Matokeo Yanga VS Azam Leo Fainali Ngao ya Jamii 2024

Yanga 4-1 Azam
  • Dakika ya 13’- Feitoto anaifungia Azam Goli la kwanza
  • Dakika ya 19′- Prince Dubeee Anasawazisha. Yanga 1-1 Azam Fc
  • Dakika ya 28′ Boka anapiga Krosi chonganishi na Yolo anajitia kamba. Yanga 2-1 Azam Fc
  • Aziz ki anaipa Yanga goli la 3
  • Kipindi cha Kwanza kimemalizika: Yanga Sc 3-1 Azam Fc

🔰𝐌𝐀𝐓𝐂𝐇𝐃𝐀𝐘🔰

  • 🏆 #Ngao ya Jamii 2024
  • ⚽️ Young Africans SC🆚Azam FC
  • 📆 11.08.2024
  • 🏟 Benjamin Mkapa
  • 🕖 Saa Moja Usiku

Angalia Hapa Kikosi Cha Yanga Vs Azam Fc Fainali Ngao ya Jamii 11/08/2024

Matokeo Yanga VS Azam Leo Fainali Ngao ya Jamii 2024

Utabiri na Hitimisho

Mchezo huu unatarajiwa kuwa wa kusisimua na wenye ushindani mkali. Timu zote mbili zina wachezaji wenye uwezo mkubwa, na zimejiandaa vyema kwa ajili ya fainali hii. Matokeo yanaweza kwenda upande wowote, lakini jambo moja ni hakika: mashabiki wa soka watapata burudani ya hali ya juu.

Je, ni Yanga watakaodumisha ubabe wao, au Azam watalipa kisasi? Jibu litapatikana leo usiku kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa!

Mapendekezo ya Mhariri

  1. Matokeo ya Simba Vs Coastal union Leo Ngao ya Jamii 11/08/2024
  2. Kikosi Cha Simba VS Coastal union Ngao ya Jamii 11/08/2024
  3. Matokeo ya Ngao ya Jamii 2024
  4. Ratiba ya Mechi za Yanga Ligi Kuu NBC 2024/2025
  5. Ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara 2024/2025 (NBC Premier league)
  6. Man City Washinda Ngao ya Jamii 2024 Baada ya Kuichapa Man United Kwa Penalti

 

Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo