Mwenyekiti wa Bodi ya Simba Ajiuzulu, Try Again ametangaza kujiuzulu

Mwenyekiti wa Bodi ya Simba Ajiuzulu, Try Again ametangaza kujiuzulu: Simba Sports Club imekumbwa na mabadiliko makubwa baada ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Salim Abdallah “Try Again” Muhene, kutangaza kujiuzulu wadhifa wake kwa hiari leo. Uamuzi huu wa kushangaza umeacha maswali mengi kuhusu mustakabali wa klabu hii kongwe nchini Tanzania.

Mwenyekiti wa Bodi ya Simba Ajiuzulu, Try Again ametangaza kujiuzulu

Mwenyekiti wa Bodi ya Simba Ajiuzulu, Try Again ametangaza kujiuzulu

Try Again alitangaza kuachia ngazi kupitia mitandao ya kijamii ya klabu, akieleza kuwa uamuzi wake unalenga “kutoa nafasi kwa klabu ya Simba kuwa na mwanzo mpya ulio bora zaidi.” Hata hivyo, hakufafanua zaidi kuhusu sababu za msingi zilizopelekea uamuzi huu.

Try Again amekuwa kiongozi muhimu katika klabu ya Simba kwa miaka saba iliyopita, akiwa amehudumu kama Mjumbe wa Bodi, Makamu Mwenyekiti, na hatimaye Mwenyekiti. Katika kipindi chake, Simba imepata mafanikio makubwa, ikiwa ni pamoja na mataji ya Ligi Kuu Tanzania Bara, Kombe la Shirikisho (ASFC), na ushiriki wa mara kwa mara katika michuano ya kimataifa.

Katika hatua ya kushangaza zaidi, Try Again amependekeza Mohammed Dewji, Mwekezaji na Rais wa Heshima wa Simba, kuchukua nafasi yake kama Mwenyekiti wa Bodi. Dewji, ambaye ni mfanyabiashara maarufu na mpenzi mkubwa wa soka, ana uzoefu mkubwa katika uongozi wa michezo na anaaminika kuwa na uwezo wa kuipeleka Simba kwenye kiwango kingine.

Je, Kujiuzulu Kutaathiri Simba?

Kujiuzulu kwa Try Again kumeibua hisia mseto miongoni mwa mashabiki wa Simba. Baadhi wana wasiwasi kuhusu mabadiliko haya ya ghafla, huku wengine wakiona kuwa ni fursa ya kuanza upya na kujenga timu imara zaidi.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Taifa Stars Yashinda 1-0 Dhidi ya Zambia, Hatua Kubwa Kuelekea Kombe la Dunia
  2. Singida Black Stars Yamteua Hussein Masanza Kama Afisa Habari Mpya
  3. Ratiba ya Kagame CECAFA Cup 2024
  4. Klabu za Tanzania Zinazoshiriki Kagame Cecafa CUp 2024
  5. Timu zitakazo shiriki CECAFA kagame Cup 2024
  6. Tetesi za Usajili simba 2024/2025
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo