Tanzania Ipo Nafasi ya Ngapi Viwango vya FIFA 2024

Tanzania Ipo Nafasi ya Ngapi Viwango vya FIFA

Kufuatia matokeo ya kuridhisha katika mechi za hivi karibuni, timu ya taifa ya Tanzania, maarufu kama Taifa Stars, imeendelea kupanda katika viwango vya ubora wa soka duniani vya FIFA. Timu hiyo imevuna pointi nne muhimu katika mechi mbili za kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) dhidi ya Ethiopia na Guinea, hali ambayo imechangia kuimarisha nafasi ya Tanzania kimataifa.

Tanzania Yapanda Nafasi Katika Viwango vya FIFA

Kulingana na viwango vya FIFA vilivyotangazwa leo septemba 19 2024, Tanzania imepanda kutoka nafasi ya 113 hadi nafasi ya 110 duniani. Hii ni baada ya ongezeko la nafasi tatu ambalo linaashiria mwenendo mzuri wa ubora wa soka la Tanzania, hasa kutokana na jitihada za wachezaji na benchi la ufundi.

Tanzania Ipo Nafasi ya Ngapi Viwango vya FIFA

Kupanda huku kunatokana na ushindi na sare zilizopatikana dhidi ya Ethiopia na Guinea, ambazo zimeongeza idadi ya pointi muhimu kwa Tanzania katika viwango vya FIFA. Mashabiki na wadau wa soka nchini wanaendelea kushuhudia ukuaji wa kiwango cha timu ya taifa, huku matumaini yakiwa makubwa kwa mafanikio zaidi katika mashindano ya kimataifa yajayo.

Hali ya Timu Nyingine za Ukanda wa Afrika Mashariki

Katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, maarufu kama CECAFA, Uganda inasalia kuwa kinara kwa sasa, baada ya kupanda kwa nafasi tano kutoka nafasi ya 95 hadi nafasi ya 90 duniani.

Kenya nayo imepanda kwa nafasi sita kutoka 108 hadi 102 duniani, ikiashiria kuwa juhudi za kuimarisha soka la nchi hiyo zinaendelea kuzaa matunda. Nchi nyingine za ukanda wa CECAFA pia zimepata maendeleo katika viwango vya FIFA, zikiwemo Sudan, Rwanda, na Burundi, ambazo zimeongeza nafasi zao kwa viwango tofauti.

Hata hivyo, baadhi ya nchi zimeshuka kwenye viwango, ikiwemo Ethiopia na Sudan Kusini. Ethiopia imeshuka kwa nafasi mbili kutoka nafasi ya 143 hadi 145, huku Sudan Kusini ikishuka kwa nafasi tatu kutoka nafasi ya 169 hadi 172 duniani.

Timu Zilizopo Juu Kidunia na Barani Afrika

Kwa upande wa viwango vya FIFA duniani, Argentina inaendelea kuongoza dunia, ikifuatiwa na Ufaransa, Hispania, England, na Brazil. Timu hizi tano zimeendelea kudhihirisha ubora wao kimataifa kwa kushinda mataji makubwa na kushiriki mashindano ya hadhi.

Barani Afrika, Morocco inaongoza kama taifa bora katika viwango vya FIFA, ikifuatiwa na Senegal, Misri, Ivory Coast, na Tunisia. Timu hizi zimeonyesha uwezo mkubwa barani na zinaendelea kuimarisha nafasi zao katika viwango vya ubora wa FIFA.

Viwango vya FIFA vinavyofuata vinatarajiwa kutangazwa tarehe 24 Oktoba 2024. Mashabiki wa soka Tanzania na kwingineko wanatazamia kuona endapo Taifa Stars itaendelea kupanda zaidi katika viwango hivyo, hasa kutokana na mfululizo wa matokeo bora waliyoanza kuyapata.

Kwa sasa, kupanda kwa nafasi ya Tanzania katika viwango vya FIFA ni ishara njema kwa maendeleo ya soka nchini, huku ikionesha kuwa juhudi za kuwekeza katika soka zinaanza kuzaa matunda.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Viwango vya FIFA Afrika 2024 Timu za Taifa
  2. Kikosi cha Al Ahli Tripoli Chawasili na Bodyguards Kibao Airport
  3. Mtasingwa Afunguka Kwanini Aliitosa Yanga
  4. Ishu ya Joshua Mutale na Jezi ya Kombe la Shirikisho CAF
  5. Refa Asiye na Uzoefu Kuchezesha Mtanange wa Simba vs Al Ahli Tripoli
  6. Elie Mpanzu Kwenye Rada za Yanga na Simba
  7. Yanga Yafanya ‘Homework’ ya Kutosha, Gamondi Apania Tiketi ya Makundi
  8. Fadlu Davids Afurahishwa na Ngome ya Ulinzi Simba
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo