Nafasi za Kazi Wizara ya Ardhi 2024 (Ajira ya Muda Mfupi)

Nafasi za Kazi Wizara ya Ardhi 2024 (Ajira ya Muda Mfupi) | Nafasi Mpya za Ajira za Muda Wizara ya Ardi

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imekuwa mstari wa mbele katika kusimamia na kudhibiti rasilimali za ardhi nchini Tanzania. Katika mwaka wa 2024, wizara hii imetangaza nafasi za ajira ya muda mfupi kwa Watanzania.

Ajira hizi ni nafasi muhimu zinazotoa fursa kwa waombaji wenye sifa stahiki kujiunga na timu ya Wizara ya Ardhi, huku wakisaidia katika shughuli za Baraza la Ardhi na Nyumba. Katika makala hii, habariforum tumekuletea taarifa za kina kuhusu nafasi mpya za kazi zilizotangazwa na wizara ya Ardi, sifa zinazohitajika, jinsi ya kutuma maombi, na manufaa unayoweza kuyapata kwa kujiunga na ajira hizi.

Nafasi za Kazi Wizara ya Ardhi 2024 (Ajira ya Muda Mfupi)

Wizara ya Ardhi imetangaza nafasi za Katibu Mahsusi Daraja la III (Personal Secretary III) zenye ajira ya muda mfupi kwa jumla ya nafasi 87. Nafasi hizi zinapatikana katika wilaya mbalimbali nchini Tanzania zikiwemo Arumeru, Bagamoyo, Dodoma, Kigoma, Mbeya, Mwanza, na wilaya nyingine nyingi. Hii ni fursa ya kipekee kwa Watanzania wenye nia ya kuchangia katika maendeleo ya taifa kupitia sekta ya ardhi.

Nafasi za Kazi Wizara ya Ardhi 2024 (Ajira ya Muda Mfupi)

Sifa za Waombaji wa Ajira ya Muda Mfupi Wizara Ya Ardhi 2024

Wizara ya Ardhi imeweka wazi sifa za msingi ambazo waombaji wanapaswa kuwa nazo ili kuzingatia maombi yao. Zifuatazo ni baadhi ya sifa muhimu zinazohitajika:

  1. Mwombaji lazima awe Mtanzania mwenye umri wa miaka 18 hadi 45.
  2. Kipaumbele kitapewa waombaji ambao ni wakazi wa wilaya ambayo nafasi inapatikana.
  3. Mwombaji anapaswa kuwa na sifa na uzoefu wa kazi za uhazili (uchapaji na utunzaji kumbukumbu), na awe na uwezo wa kufanya kazi chini ya uangalizi mdogo.

Sifa za Kitaaluma

  1. Mwombaji awe amehitimu kidato cha IV au VI na kuwa na cheti cha uhazili kutoka kwenye Chuo cha Utumishi wa Umma au chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.
  2. Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta na kufaulu mitihani ya hatua ya tatu ya uhazili kwa Kiswahili na Kiingereza (hatimkato) kwa kiwango cha maneno 80 kwa dakika.

Kazi na Majukumu

Waombaji watakaoajiriwa watakuwa na majukumu mbalimbali katika ofisi za Baraza la Ardhi na Nyumba za wilaya. Baadhi ya majukumu hayo ni pamoja na:

  1. Kuchapa nyaraka na taarifa mbalimbali zikiwemo hukumu na mienendo ya mashauri.
  2. Kupokea wageni na kuwaelekeza kwa huduma wanazohitaji.
  3. Kutunza taarifa za matukio, miadi, na safari za kazi za msimamizi.
  4. Kusimamia usafi na uendeshaji wa ofisi kwa ujumla.
  5. Kufanya kazi nyinginezo zitakazoelekezwa na msimamizi kulingana na miongozo ya utumishi wa umma.

Maelezo Mengine Kuhusu Ajira Hizi

Ajira hii ni ya muda mfupi (Temporary Employment) ambapo waombaji watakaofanikiwa wataajiriwa kwa muda uliopangwa kwa mujibu wa mikataba. Ngazi ya mshahara itakuwa katika kiwango cha TGS B 1, na masharti mengine ya kazi yatafuata kanuni za utumishi wa umma nchini.

Jinsi ya Kutuma Maombi Nafasi za Kazi Wizara ya Ardhi (Ajira ya Muda Mfupi)

Waombaji wanahitajika kuwasilisha maombi yao moja kwa moja kwenye Ofisi za Baraza la Ardhi na Nyumba katika wilaya husika ambako nafasi zimetangazwa. Maombi hayo yanapaswa kuambatana na:

  • Maelezo binafsi yanayojitosheleza (CV) pamoja na namba za simu na anuani sahihi.
  • Nakala za vyeti vya taaluma (kidato cha IV au VI) na cheti cha kuzaliwa.
  • Picha mbili za pasipoti za hivi karibuni zikiwa na jina la mwombaji kwa nyuma.
  • Hati za matokeo ya mitihani (testimonial au provisional results) hazitakubaliwa.

Mwisho wa kuwasilisha maombi ni tarehe 26 Septemba 2024, saa 9:30 mchana. Waombaji wanatakiwa kuelekeza maombi yao kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, L.P. 2908, Dodoma.

Faida za Kuajiriwa Wizara ya Ardhi

Kuajiriwa kwenye Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kunaleta fursa kadhaa muhimu. Kwanza, ni nafasi nzuri ya kujifunza na kupata uzoefu katika sekta ya umma, hususan katika kusimamia masuala ya ardhi na nyumba.

Pili, waombaji wanaweza kutumia nafasi hii kujenga mtandao wa kitaaluma, kujiendeleza kitaaluma, na kuongeza fursa za ajira katika siku zijazo. Aidha, ajira hii itawawezesha watumishi kupata ujuzi muhimu wa kiutawala, ambao utakuwa na manufaa kwao katika shughuli za kiofisi na utumishi wa umma kwa ujumla.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Nafasi Mpya za Kazi Ualimu MDAs NA LGAs 17-09-2024
  2. Taarifa Muhimu kwa Waombaji Kazi za Ualimu AJira Portal 14 September 2024
  3. Kuhakiki Mwajiri Ajira Portal (Employer Confirmation): Mwongozo Kamili kwa Walimu
  4. Majina ya Walioitwa kwenye Usaili Ajira Portal 2024
  5. Jinsi ya Kubadili Kituo Cha Usaili Ajira Portal
  6. Ajira Mpya za Walimu Tanzania 2024: Nafasi 11,015 Zatangazwa, Maombi Hadi Agosti 2
  7. Majina ya Walioitwa Kwenye Usaili Tume ya Utumishi wa Mahakama (JSC) Septemba 11 2024
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo