Majina ya Walioitwa Kwenye Usaili Tume ya Utumishi wa Mahakama (JSC) Septemba 11 2024

Majina ya Walioitwa Kwenye Usaili Tume ya Utumishi wa Mahakama (JSC)

Katika juhudi zake za kuimarisha mfumo wa utoaji haki nchini Tanzania, Tume ya Utumishi wa Mahakama (Judicial Service Commission – JSC) imeendelea na mchakato wa kuajiri watumishi wapya. Tume imetoa tangazo la majina ya walioitwa kwenye usaili wa ana kwa ana na usaili wa vitendo kwa Kada mbalimbali kama vile Afisa Tehama II, Mwandishi Mwendesha Ofisi II, na Dereva II.

Majina ya walioitwa kwenye usaili, pamoja na vituo na tarehe husika, yameorodheshwa kwenye tovuti rasmi za Mahakama ya Tanzania (www.judiciary.go.tz) na Tume ya Utumishi wa Mahakama (www.jsc.go.tz). Wasailiwa wote wameelekezwa kufika kwenye vituo vilivyopangwa kwa muda uliotajwa, na usaili utaanza kuanzia saa 2:00 asubuhi.

Majina ya Walioitwa Kwenye Usaili Tume ya Utumishi wa Mahakama (JSC) Septemba 11 2024

Angalia Majina ya Walioitwa Kwenye Usaili Tume ya Utumishi wa Mahakama (JSC) Septemba 11 2024 Kupitia Kiungo kilichopo chini

TANGAZO_KUITWA KWENYE USAILI AWAMU YA PILI_12_09_2024_FINAL1

Bofya Hapa Kupakua Pdf

Kwa wale ambao majina yao yapo kwenye orodha ya majina ya walioitwa kwenye usaili katika tangazo la Tume ya Utumishi wa Mahakama, utaratibu ni kama ifuatavyo:

  • Usaili wa Vitendo: Usaili huu unahusisha mtihani wa vitendo kwa Kada zilizoainishwa, kama vile Afisa Tehama na Dereva, ambapo ujuzi wa kitaalamu na uwezo wa kiufundi utapimwa. Wasailiwa watahitajika kuonyesha umahiri wao kupitia majaribio halisi yanayohusiana na nafasi wanayoomba.
  • Usaili wa Ana kwa Ana: Baada ya usaili wa vitendo, watakaofaulu wataendelea na usaili wa ana kwa ana ambapo watapimwa uwezo wao wa kiakili, ujuzi wa taaluma, na ustadi wa mawasiliano. Usaili huu utajumuisha maswali ya moja kwa moja ambayo yatatoa fursa kwa waombaji kuelezea kwa kina sifa zao.

Nini Cha Kufanya Kabla ya Usaili

Wasailiwa wanashauriwa kufanya maandalizi yafuatayo kabla ya kuhudhuria usaili:

  1. Vyeti Halisi: Wahakikishe wanakuwa na vyeti vyote halisi vya Elimu, Taaluma, na vyeti vingine muhimu kama cheti cha kuzaliwa.
  2. Vituo Vilivyopangiwa: Ni muhimu kuhudhuria usaili kwenye kituo kilichopangiwa, kwa kuwa usaili hautafanyika nje ya vituo hivyo.
  3. Saa ya Kufika: Wasailiwa wote wanapaswa kufika mapema kabla ya saa 2:00 asubuhi kwa ajili ya maandalizi ya usaili.

Wale Ambao Majina Yao Hayapo

Kwa wasailiwa ambao hawajapata nafasi ya kuendelea na hatua ya pili ya usaili, hawakufaulu hatua ya kwanza ya mchakato. Hata hivyo, wanashauriwa kuendelea kufuatilia nafasi nyingine za ajira zinazotangazwa na Tume kwa nyakati tofauti.

Kwa Taarifa na Maelezo Zaidi

Kwa wale wanaohitaji maelezo zaidi au ufafanuzi kuhusu tangazo hili, wanakaribishwa kuwasiliana na Tume ya Utumishi wa Mahakama kupitia:

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Majina ya Walioitwa kwenye Usaili Ajira Portal 2024
  2. Nafasi Za Kazi Mamlaka Ya Usimamizi Wa Wanyamapori Tanzania (Tawa) 01-09-2024
  3. Nafasi Za Kazi Taasisi Ya Utafiti Wa Misitu Tanzania (Tafori) 01-09-2024
  4. Majina ya Walioitwa Kwenye Usaili Kada za Afya MDAs & LGAs 28-08-2024
  5. Majina Ya Walioitwa Kwenye Usaili Mteknolojia Msaidizi Daraja La II 29/08/2024
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo