Tetesi za Usajili Ligi Kuu ya NBC 2026/2027 Tanzania

Tetesi za Usajili Ligi Kuu ya NBC 2026/2027 Tanzania | Usajili Mpya Ligi Kuu Tanzania Bara

Soko la usajili wa Ligi Kuu ya NBC limeanza kupamba moto mapema, huku klabu zikianza kusuka vikosi vyao kuelekea msimu wa 2026/2027. Taarifa zinazoibuka kila siku zinaonyesha wazi kuwa msimu ujao utakuwa na ushindani mkali, si uwanjani tu bali hata kwenye usajili.

Kuanzia Kariakoo hadi Singida, kila timu inaonekana kuwa na malengo yake wengine wanajenga upya, wengine wanaboresha maeneo machache, na wengine wanapambana kubaki na wachezaji wao muhimu.


Tetesi za Usajili Ligi Kuu ya NBC 2026/2027 Tanzania

Vita ya Kariakoo yaanza mapema

Moja ya ishu kubwa kwenye usajili msimu huu ni ya Keletso Makgalwa.

Mwanzoni kabisa, ilielezwa kuwa Yanga ndiyo ilikuwa mbele kwenye dili hilo. Mazungumzo yalikuwa yameenda mbali na ilionekana wazi kuwa ni suala la muda tu kumalizana.

Lakini mambo yakabadilika ghafla.

Taarifa za baadaye zikaanza kueleza kuwa Simba imeingilia kati na kufanikisha dili hilo. Hii inaonyesha wazi namna ambavyo Simba na Yanga zinavyokabiliana hata kabla ya msimu kuanza.

Katika kipindi hicho hicho, Yanga ilipoteza nafasi ya kumsajili beki Nasri Kombo, baada ya mchezaji huyo kuamua kuongeza mkataba TRA United.


Simba SC: inaongeza nguvu kwa waliothibitisha uwezo

Simba imeamua kwenda tofauti kidogo msimu huu kwa kulenga wachezaji wanaoijua vizuri ligi ya ndani.

Majina yanayotajwa kujiunga ni:

  • Nathaniel Chilambo, aliyemaliza mkataba Azam
  • Ramadhan “Chobwedo” Salum, kiungo wa TRA
  • Keletso Makgalwa, winga kutoka Afrika Kusini

Hii inaonyesha Simba inalenga kupata wachezaji ambao hawatahitaji muda mrefu kuzoea mazingira.

Upande wa wanaoondoka nao upo wazi:

  • Chamou Karaboue tayari ameondoka kwenda Iraq
  • Anicet Oura anatajwa kuvutiwa na klabu za nje
  • Hussein Abel hana nafasi kwenye mipango ya kikosi

Kwa hiyo Simba haiongezi tu pia inapunguza.


Yanga SC: inachagua kwa umakini

Kwa upande wa Yanga, mambo yanaenda kwa utulivu lakini kwa umakini mkubwa.

Katika safu ya ulinzi, Mohamed Mussa wa Mashujaa ni mmoja wa wachezaji ambao Yanga inamsukuma kwa nguvu. Mazungumzo yamefika mbali, kilichobaki ni kukamilisha taratibu za mwisho kati ya klabu hizo mbili.

Mbali na hapo, Yanga inaendelea kumtazama:

  • Juma Abushiri “Chuga”
  • Viungo kama Pipino na Gego

Hawa bado wako kwenye hatua ya kufuatiliwa, hakuna makubaliano yaliyothibitishwa.

Kwa upande wa wanaoondoka:

  • Prince Dube tayari ameondoka na kujiunga na Hardrock FC
  • Sure Boy sasa ni mchezaji huru, akihusishwa na JKT na Mashujaa

Yanga inaonekana haikurupuki inachukua muda kabla ya kufanya maamuzi.


Singida Black Stars: haiji kushiriki, inakuja kupambana

Singida Black Stars ni moja ya timu zinazofanya mambo makubwa kimya kimya.

Kwanza kabisa, imeanza kwa kuhakikisha inalinda msingi wake:

  • Metacha Mnata ameongezewa mkataba wa miaka 3

Kwenye usajili:

  • Jephte Kitambala yuko karibu kujiunga
  • Yona Amosi ameripotiwa kukubaliana na klabu
  • Mussa Hassan “Mbappe” bado mambo yake hayajakaa sawa kabisa

Lakini changamoto ipo upande wa kuzuia wachezaji kuondoka:

  • Mosi Nduwumwe anawindwa na Simba na Yanga

Singida kwa sasa:

inajenga na wakati huo huo inalinda kile ilichonacho


Azam FC: mabadiliko makubwa yanaendelea

Azam inaonekana kubadilisha sura ya kikosi chake.

Majina yanayotajwa kuingia:

  • Hassan Mubiru
  • Henri Stanic
  • Jeancy Mukuene

Hawa wote wako kwenye hatua za mwisho au mazungumzo ya karibu.

Lakini upande wa kutoka unaonekana kuwa mkubwa:

  • Nathaniel Chilambo → Simba
  • Jephte Kitambala → Singida
  • Yoro Diaby → hatma yake bado haijaeleweka

Hii inaonyesha Azam haiongezi tu wachezaji, bali inabadilisha muundo wa timu.


TRA United: haitaki kuyumba

TRA imeamua kulinda kikosi chake kwa nguvu.

  • Nasri Kombo ameongeza mkataba wa miaka 2
  • Mzamiru Yassin ameendelea kubaki

Hii imezuia moja kwa moja baadhi ya mipango ya klabu nyingine.

Hata hivyo, kuna uwezekano wa kupoteza:

  • Chobwedo kuelekea Simba
  • Nouma ambaye anahusishwa na Singida

Mashujaa na JKT: nazo zinaongeza nguvu

Mashujaa imeanza kufanya kazi mapema:

  • Hassan Kabunda
  • Abdallah Mfuko

Wote wameripotiwa kumalizana na klabu hiyo, ingawa bado hawajatangazwa rasmi.

Kwa upande wa JKT Tanzania:

  • Constantine Malimi
  • Ismail Mhesa

Nao wameripotiwa kujiunga na klabu hiyo.


Timu zilizopanda daraja: zinajipanga kubaki

Kagera Sugar na Geita Gold zimeanza kuonyesha mapema nia yao ya kubaki ligi kuu.

  • Kagera imemsajili Dickson Mhilu
  • Geita imehusishwa na Datius Peter
  • Pius Buswita anawindwa na Geita na Coastal

Hii inaonyesha wazi kuwa timu hizi zinataka kujiweka salama mapema.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Tetesi Za Usajili Yanga 2026/2027: Usajili Mpya, Wanaotajwa na Wanaoweza Kuondoka
  2. CV Ya Manqoba Mngqithi Kocha Mpya wa Yanga 2026/2027
  3. Rasmi: Yanga Yamtambulisha Manqoba Mngqithi Kuwa Kocha Mkuu
  4. Hili Apa Kundi la Simba CECAFA Kagame Cup 2026
  5. Makundi CECAFA Kagame Cup 2026: Simba na Singida Black Stars Kundi B
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo