Yanga Yamsajili Rasmi Aziz Andabwile: Mkataba wa Miaka miwili, Kiungo Mpya Jangwani

Yanga Yamsajili Rasmi Aziz Andabwile: Mkataba wa Miaka miwili, Kiungo Mpya Jangwani

Katika hatua inayoendelea kuonyesha nia ya kutawala soka la Tanzania na Afrika Mashariki, mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga SC, wamekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji mwenye kipaji cha hali ya juu, Aziz Andabwile. Usajili huu wa kusisimua umetangazwa rasmi leo tarehe 9 Julai, 2024, kupitia kurasa za mitandao ya kijamii za klabu hiyo.

Yanga Yamsajili Rasmi Aziz Andabwile: Mkataba wa Miaka miwili, Kiungo Mpya Jangwani

Aziz Andabwile, mwenye umri wa miaka 24, anatua Yanga SC akiwa na uzoefu mkubwa wa kucheza soka la ushindani, akitokea Fountain Gate FC (zamani ikijulikana kama Zaman Singida Fountain Gate). Kiungo huyu mshambuliaji amejizolea sifa kutokana na uwezo wake wa kuchezesha timu, kupiga pasi za mwisho zenye macho, na kufunga mabao ya kusisimua. Uwepo wake unatarajiwa kuongeza nguvu zaidi katika safu ya ushambuliaji ya Yanga SC.

Yanga Yamsajili Rasmi Aziz Andabwile: Mkataba wa Miaka miwili, Kiungo Mpya Jangwani

Angalia Video ya Utambulisho wa Aziz Andambwile Yanga

Mkataba wa miaka miwili uliosainiwa na Andabwile unaonyesha imani kubwa ambayo Yanga SC inayo kwake. Klabu inaamini kwamba kiungo huyu atakuwa mchezaji muhimu katika kikosi chao na kuchangia pakubwa katika mafanikio zaidi, ikiwemo kutetea ubingwa wa Ligi Kuu na kufanya vizuri katika michuano ya kimataifa.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Tetesi za Usajili simba 2024/2025
  2. Tetesi za Usajili Ligi Kuu Tanzania Bara 2024/2025
  3. FIFA Yaiondolea Yanga Adhabu ya Kufungiwa Kusajili
  4. Dirisha la Usajili Ligi Kuu Tanzania kufunguliwa Juni 15 hadi Agosti 15, 2024
  5. Tetesi za Usajili Yanga: Okrah Kwenye Rada za Kuondoka Yanga? Habari Kamili
  6. Jinsi Ya Kuangalia Usajili Wa Namba ya Simu
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo