Washindi wa Ngao ya Jamii Miaka Yote

Washindi wa Ngao ya Jamii Miaka Yote | Ngao ya jamii simba imechukua mara ngapi, Ngao ya jamii Yanga imechukua mara ngapi, Historia ya Washindi wa Ngao Ya Jamii

Michezo ya Ngao ya Jamii imekuwa moja ya mashindano muhimu katika soka la Tanzania, ikileta pamoja klabu bora zinazoshindana kuashiria mwanzo wa msimu mpya wa ligi. Ngao ya Jamii imeanzishwa kwa lengo la kukuza mshikamano na kuleta furaha kwa mashabiki wa soka nchini. Hapa tunakuletea historia na washindi wa kombe hili tangu kuanzishwa kwake.

Historia ya Ngao ya Jamii

Ngao ya Jamii ilianzishwa mwaka 2001, ikianza kwa mchezo wa kukata na shoka kati ya watani wa jadi, Simba na Yanga. Katika mchezo huo wa kwanza, Yanga waliibuka washindi kwa kuifunga Simba 2-1. Mabao ya Yanga yalifungwa na Edibily Lunyamila na Ally Yussuph ‘Tigana’, huku bao pekee la Simba likifungwa na Steven Mapunda ‘Garincha’.

Mashindano haya hayakuchezwa tena kwa miaka kadhaa hadi yaliporejea mwaka 2009. Tangu wakati huo, yameendelea kuwa kipimo cha kuashiria mwanzo wa msimu mpya wa ligi, yakihusisha klabu ambazo zimefanya vizuri katika msimu uliopita wa ligi kuu ya Tanzania.

Washindi wa Ngao ya Jamii Miaka Yote

Orodha ya Washindi wa Ngao ya Jamii Miaka Yote

Mwaka Mshindi Matokeo
2001 Yanga SC 2-1 Simba SC
2009 Mtibwa Sugar 1-0 Yanga SC
2010 Yanga SC 3-1 Simba SC (Pen)
2011 Simba SC 2-0 Yanga SC
2012 Simba SC 3-2 Azam FC
2013 Yanga SC 1-0 Azam FC
2014 Yanga SC 3-0 Azam FC
2015 Yanga SC 8-7 Azam FC (Pen)
2016 Azam FC 4-1 Yanga SC (Pen)
2017 Simba SC 5-4 Yanga SC (Pen)
2018 Simba SC 2-1 Mtibwa Sugar
2019 Simba SC 4-2 Azam FC
2020 Simba SC 2-0 Namungo FC
2021 Yanga SC 1-0 Simba SC
2022 Yanga SC 2-1 Simba SC
2023 Simba SC 3-1 Yanga SC (Pen)

Ngao ya Jamii Simba Imechukua Mara Ngapi?

Simba imekuwa na mafanikio makubwa katika mashindano ya Ngao ya Jamii, ikiwa imechukua taji hilo mara nyingi. Simba imeshinda Ngao ya Jamii mara kumi (10), ikionyesha uwezo wao mkubwa na ushindani katika soka la Tanzania. Ushindi wao wa kwanza ulikuja mwaka 2011 walipoifunga Yanga 2-0, na ushindi wao wa hivi karibuni ulikuwa mwaka 2023 waliposhinda dhidi ya Yanga kwa penalti.

Ngao ya Jamii Simba Imechukua Mara Ngapi?

Ngao ya Jamii Yanga Imechukua Mara Ngapi?

Yanga pia imeonyesha ubora wao katika mashindano ya Ngao ya Jamii, ambapo imeshinda taji hilo mara saba (7). Ushindi wao wa kwanza ulikuwa mwaka 2001 walipoifunga Simba 2-1 katika mchezo wa kwanza wa Ngao ya Jamii. Ushindi wao wa hivi karibuni ulikuwa mwaka 2022 waliposhinda dhidi ya Simba kwa mabao 2-1. Mafanikio haya yanaashiria jinsi Yanga ilivyo imara katika mashindano haya.

Ngao ya Jamii Yanga Imechukua Mara Ngapi?

Utawala wa Simba na Yanga

Kama inavyoonekana kwenye orodha ya washindi, Simba na Yanga ndiyo klabu zinazotawala katika mashindano haya. Ushindani wao umeleta burudani kubwa kwa mashabiki na kuimarisha soka la Tanzania.

Kwa upande mwingine, klabu ya Azam na Mtibwa Sugar nazo zimeweza kuonyesha ushindani kwa kushinda mara moja kila moja. Ushindi wa Azam dhidi ya Yanga mwaka 2016, ulikuwa wa kuvutia zaidi kwani waliifunga Yanga kwa penalti 4-1.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Rekodi za Simba na Yanga Kufungana
  2. TFF Kutoa Adhabu Kali kwa Maofisa Habari Wachekeshaji
  3. TFF Yatoa Onyo Kali Kwa Wanaojihusisha na Ushirikina Katika Mechi za Mpira
  4. Ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara 2024/2025 (NBC Premier league)
  5. Mechi ya Yanga Vs Simba Kesho Saa Ngapi, Wapi, na Jinsi ya Kuitazama
  6. Waamuzi Mechi ya Yanga Vs Simba 08/08/2024
  7. Straika wa Mali Amara Bagayoko Atua Coastal Union
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo