Viwango vya FIFA Afrika 2024 Timu za Taifa

Orodha Viwango Vipya vya FIFA Ubora wa Soka Duniani September 2024 | Viwango vya FIFA Afrika 2024 Timu za Taifa

Timu za taifa za Afrika zimeendelea kuonyesha uwezo wao mkubwa kwenye viwango vya FIFA ambavyo vimetangazwa hii leo septemba 19 2024. Nchi kadhaa zimepanda juu kutokana na mafanikio ya hivi karibuni kwenye mashindano ya kimataifa, huku nyingine zikishuka kutokana na matokeo yasiyokuwa mazuri. Viwango hivi vinachangia sana kuelezea nguvu za timu za taifa kwenye ulimwengu wa soka.

Timu Zinazoongoza Afrika

Kwa upande wa bara la Afrika, Morocco inaendelea kushikilia nafasi ya juu, ikiwa katika nafasi ya 14 duniani kwa alama 1676.14. Mafanikio ya timu hii yanatokana na matokeo mazuri kwenye mashindano ya kimataifa, ikiwemo kufika hatua za juu kwenye Kombe la Dunia.

Nchi nyingine zinazofuata katika nafasi za juu barani Afrika ni Senegal (nafasi ya 21), Misri (nafasi ya 31), Ivory Coast (nafasi ya 33), na Tunisia (nafasi ya 36). Hizi timu zimeonyesha ustadi wa hali ya juu kwenye mashindano ya Afrika na kimataifa.

Tanzania na Timu Nyingine za Afrika Mashariki

Tanzania, kupitia timu yake ya mpira wa miguu kwa wanaume Taifa Stars, imepanda hadi nafasi ya 110 duniani, kutoka 113, ikiwa na jumla ya pointi 1188.24​. Kupanda huku kunachangiwa na matokeo mazuri ambayo yamepatikana katika mechi kadhaa za kufuzu mashindano ya AFCON, dhidi ya timu za Ethiopia na Guinea.

Uganda imepiga hatua kubwa kwa kupanda nafasi tano hadi kufikia nafasi ya 90, huku Kenya nayo ikipanda hadi nafasi ya 102 kutoka 108​. Timu nyingine za ukanda wa Afrika Mashariki zimeendelea kuonyesha maendeleo katika viwango vya FIFA, kama vile Sudan ambayo imepanda hadi nafasi ya 120, Rwanda nafasi ya 130, na Burundi nafasi ya 136.

Nchi Zinazoongoza Duniani

Kwa ngazi ya dunia, Argentina bado inaongoza orodha ya FIFA, ikifuatiwa na Ufaransa, Hispania, England, na Brazil. Kwa upande wa Afrika, Morocco inaongoza, ikifuatiwa na Senegal, Misri, Ivory Coast, na Tunisia. Timu hizi zimeonyesha uimara kwenye mashindano makubwa, na zimeendelea kudumisha viwango vya juu vya ubora.

Viwango vya FIFA Afrika 2024 Timu za Taifa

Viwango vya FIFA Afrika 2024 Timu za Taifa

Nafasi Afrika Nafasi Duniani Timu ya Taifa Pointi  za Sasa Pointi Msimu Ulopitra
1 14 Morocco 1676.14 1669.44
2 21 Senegal 1620.87 1623.34
3 31 Egypt 1515.64 1502.34
4 33 Côte d’Ivoire 1509.12 1499.69
5 36 Tunisia 1504.86 1494.06
6 39 Nigeria 1498.02 1498.93
7 41 Algeria 1486.03 1474.13
8 53 Cameroon 1458.51 1458.47
9 54 Mali 1455.16 1456.74
10 58 Congo DR 1416.91 1400.93
11 59 South Africa 1415.07 1415.15
12 63 Burkina Faso 1387.5 1375.16
13 65 Cabo Verde 1379.17 1380.53
14 70 Ghana 1360.43 1381.25
15 82 Guinea 1298.3 1324.8
16 84 Gabon 1292.88 1288.45
17 85 Angola 1281.09 1255.65
18 89 Benin 1257.69 1254.18
19 90 Uganda 1257.64 1242.96
20 93 Zambia 1252.79 1249.54
21 94 Equatorial Guinea 1250.57 1260.5
22 99 Mozambique 1226.03 1208.87
23 102 Kenya 1208.96 1197.73
24 105 Namibia 1201.3 1221.42
25 108 Madagascar 1196.56 1203.66
26 110 Tanzania 1188.24 1174.99
27 112 Mauritania 1179.04 1177.5
28 115 Guinea-Bissau 1166.02 1168.49
29 117 Congo 1160.33 1162.73
30 118 Comoros 1159.64 1159.84
31 119 Togo 1158.81 1158.7
32 120 Sudan 1154.5 1152.29
33 121 Libya 1153.97 1165.73
34 124 Zimbabwe 1134.99 1126.15
35 125 Sierra Leone 1134.26 1149.4
36 127 Niger 1132.39 1139.21
37 128 Central African Republic 1130.7 1129.3
38 130 Rwanda 1123.32 1114.15
39 133 Malawi 1117.42 1137.83
40 135 The Gambia 1109.05 1112.55
41 136 Burundi 1101.79 1091.24
42 143 Liberia 1064.97 1067.05
43 145 Ethiopia 1063.44 1066.16
44 147 Botswana 1050.15 1063.64
45 153 Lesotho 1034.02 1046.54
46 159 Eswatini 1012.17 1025.28
47 172 South Sudan 967.83 980.02
48 177 Chad 932.44 929.97
49 178 Mauritius 927.57 927.94
50 190 São Tomé and Príncipe 878.09 878.09
51 192 Djibouti 875.13 875.13
52 201 Seychelles 831.19 831.19
53 202 Somalia 829.81 829.81

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Kikosi cha Al Ahli Tripoli Chawasili na Bodyguards Kibao Airport
  2. Mtasingwa Afunguka Kwanini Aliitosa Yanga
  3. Ishu ya Joshua Mutale na Jezi ya Kombe la Shirikisho CAF
  4. Refa Asiye na Uzoefu Kuchezesha Mtanange wa Simba vs Al Ahli Tripoli
  5. Elie Mpanzu Kwenye Rada za Yanga na Simba
  6. Yanga Yafanya ‘Homework’ ya Kutosha, Gamondi Apania Tiketi ya Makundi
  7. Fadlu Davids Afurahishwa na Ngome ya Ulinzi Simba
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo