Vituo Vya Kununua Tiketi za Mechi ya Yanga Vs KMC 29.09.2024

Vituo Vya Kununua Tiketi za Mechi ya Yanga Vs KMC 29.09.2024 | Wanapouza Tiketi za Mechi ya Yanga vs KMC

Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara Yanga SC itakutana na KMC FC katika mechi mtanange wa kukatana shoka jumapili ya tarehe 29 Septemba 2024. Mechi hii itapigwa katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi kuanzia saa 3:00 usiku. Yanga SC, itaingia uwanjani ikiwa na morali ya ushindi baada ya kumaliza na matokeo mazuri dhidi ya Kagera Sugar na KenGold. Hii inatarajiwa kuwa mechi ya kuvutia, na mashabiki wa soka nchini Tanzania wanatarajia kuona burudani ya kiwango cha juu.

Kuelekea mechi hii, ni muhimu kwa mashabiki kujipatia tiketi mapema ili kuepuka usumbufu wa dakika za mwisho. Katika makala hii, tunakuletea vituo rasmi vya kununua tiketi kwa ajili ya mechi ya Yanga SC dhidi ya KMC. Pia, utapata maelezo ya viingilio vya tiketi.

Vituo Vya Kununua Tiketi za Mechi ya Yanga Vs KMC 29.09.2024

  1. Young Africans – Jangwani
  2. Vunja Bei – Dar Es Salaam Shops
  3. T-Money Ltd – Kigamboni
  4. Gitano Samweli – Mbagala Zakiem
  5. Khalfan Mohamed – Ilala
  6. Lampard Electronics
  7. Godwin Fredy – Geita
  8. Twisty Investment – Geita
  9. Gwambina Lounge – Gwambina
  10. Karoshy Pamba – Dar Live (Zakhiem)
  11. Antonio Service – Sinza, Kivukoni
  12. Tumpe Kamwela – Kigamboni
  13. Sovereign – Kinondoni Makaburini
  14. View Blue Skyline – Mikocheni
  15. Mkaluka Traders – Machinga Complex
  16. New Tech General Traders – Ubungo
  17. Sabana Business – Mbagala Maji Matitu
  18. Juma Burrah – Kivukoni
  19. Juma Burrah – Msimbazi
  20. Alphan Hinga – Ubungo
  21. Mtemba Service Co – Temeke
  22. Jackson Kimambo – Ubungo
  23. Shirima Shop – Leaders

Vituo Vya Kununua Tiketi za Mechi ya Yanga Vs KMC 29.09.2024

Bei za Tiketi

Kwa wale ambao wanapanga kuhudhuria mechi hii, viingilio vya tiketi vimegawanywa katika makundi tofauti ili kutoa nafasi kwa kila shabiki kufurahia mchezo. Viingilio ni kama ifuatavyo:

  • Mzunguko: TZS 5,000
  • VIP B: TZS 10,000
  • VIP A: TZS 20,000

Mashabiki wa Yanga wana kila sababu ya kujitokeza kwa wingi kwenye mechi hii ya kihistoria. Pamoja na mafanikio yao msimu uliopita, Yanga imeonesha kuwa na kikosi imara kinachoweza kutoa burudani ya hali ya juu. Pia, KMC ni timu inayokuja kwa nguvu licha ya changamoto katika mechi zilizopita, hivyo mashabiki wanatarajia pambano kali.

Jinsi ya Kujipanga kwa Mechi Hii

  • Nunua Tiketi Mapema: Kuepuka msongamano siku ya mechi.
  • Valia Nguo za Timu: Mashabiki wa Yanga watatakiwa kuvaa rangi za kijani na njano kuonesha umoja na kuhamasisha wachezaji.
  • Fika Uwanjani Mapema: Ili kuepuka usumbufu wa kuingia uwanjani.

Mapendekezo ya Mhariri:

Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo