Singida Black Stars Yafikia Makubaliano na Mwenda

Singida Black Stars Yafikia Makubaliano na Mwenda

Klabu ya Singida Black Stars imemaliza mvutano na beki wao mpya, Israel Mwenda, baada ya kufikia makubaliano ya kifedha ambayo yatawezesha mchezaji huyo kujiunga rasmi na kikosi cha timu hiyo. Mvutano huo ulitokana na madai ya mchezaji kutaka kulipwa kiasi kilichobakia cha fedha ya usajili.

Mwenda, ambaye alisajiliwa na Singida Black Stars hivi karibuni kutoka Simba SC, alikua bado hajajiunga na timu yake mpya licha ya kukamilisha taratibu zote za kuondoka Msimbazi. Hii ilitokea baada ya Mwenda kutokuwa tayari kuripoti kambini hadi pale atakapomaliziwa fedha za usajili, kiasi ambacho kilikua Sh 60 milioni.

Awali, Singida Black Stars walithibitisha kuwa hawajamlipa Mwenda fedha zote za usajili kutokana na makubaliano ya kimkataba kati ya pande hizo mbili, ambayo yanasema kiasi hicho cha fedha kingelipwa baadaye baada ya mchezaji kuanza kuichezea klabu hiyo. Hata hivyo, hali hii ilisababisha sintofahamu, huku Singida BS ikimpa Mwenda saa 24 kuripoti kambini au kuilipa klabu hiyo Sh 500 milioni endapo angevunja mkataba.

Akizungumza kuhusu suala hilo, Ofisa Habari wa Singida BS, Hussein Massanza, alieleza kuwa uongozi wa klabu umefanya mawasiliano na wawakilishi wa mchezaji, na hatimaye kufikia suluhu. Wawakilishi wa Mwenda wamekubali kulipa kiasi cha Sh 60 milioni kinachodaiwa ili beki huyo aweze kuanza rasmi kuichezea timu hiyo.

Singida Black Stars Yafikia Makubaliano na Mwenda

Makubaliano ya Pande Zote

Massanza alisema, “Tumepokea barua kutoka kwa wawakilishi wa mchezaji, wakikubali kulipa Sh 60 milioni ili Mwenda aweze kujiunga nasi. Tunawapongeza kwa hatua hiyo na tunatarajia kuona mchezaji anaripoti kambini haraka iwezekanavyo.”

Singida Black Stars imeonyesha utayari wa kumaliza suala hilo kwa amani, huku wakisisitiza kuwa malipo ya fedha za usajili yatafanyika kwa mujibu wa makubaliano ya awali ya mkataba. Uongozi wa klabu unatarajia Mwenda atajiunga na timu hiyo bila kuchelewa zaidi, ili aweze kuanza maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu ya NBC Tanzania.

Tamko la Msimamizi wa Mwenda

Kwa upande mwingine, msimamizi wa Israel Mwenda, Herve Tra Bi, alithibitisha kuwa wamefikia makubaliano na klabu ya Singida Black Stars. Alisema wako tayari kulipa Sh 60 milioni, kwa mujibu wa makubaliano ya mkataba, huku akithibitisha kuwa kiasi hicho kitalipwa na Singida baadaye, kama ilivyoainishwa katika mkataba wa awali.

Mwenda sasa anatarajiwa kuungana na wachezaji wenzake kambini haraka iwezekanavyo, baada ya sintofahamu hiyo kumalizika. Mashabiki wa Singida Black Stars wana matarajio makubwa kwa beki huyo mpya, ambaye anajulikana kwa uchezaji wake wa nguvu na uwezo wa kudhibiti safu ya ulinzi.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Picha za Jezi Mpya za Dodoma Jiji 2024/2025
  2. Wachezaji Sita wa Uingereza Watajwa Kwenye Orodha ya Ballon d’Or 2024
  3. Moloko Atoa Maoni Yake Baada ya Mchezo wa Stars na Ethiopia
  4. Wachezaji Wanaowania Tuzo ya Ballon d’Or 2024
  5. Ratiba ya Mechi za Leo 05 September 2024
  6. Kocha Gamondi Amshawishi Mzize Kubaki Yanga
  7. Nitabaki Yanga Mpaka Rais Hersi Asema Inatosha – Aucho
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo