Refa Asiye na Uzoefu Kuchezesha Mtanange wa Simba vs Al Ahli Tripoli

Refa Asiye na Uzoefu Kuchezesha Mtanange wa Simba vs Al Ahli Tripoli

Simba SC inatarajia kukutana na Al Ahli Tripoli kwenye mchezo wa marudiano wa raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika, ambao unatarajiwa kufanyika Jumapili, saa 10:00 jioni katika Uwanja wa Benjamin Mkapa. Hata hivyo, kinachozua mjadala mkubwa ni uteuzi wa mwamuzi Abdoulaye Manet kutoka Guinea, ambaye hana uzoefu mkubwa katika michezo ya kimataifa.

Abdoulaye Manet: Safari ya Kuanza Majukumu ya Kimataifa

Refa Asiye na Uzoefu Kuchezesha Mtanange wa Simba vs Al Ahli Tripoli

Manet, mwenye umri wa miaka 34, alipata beji ya FIFA mwaka 2020, na alianza rasmi kuteuliwa kuchezesha mechi za kimataifa mnamo Februari 21, 2021. Katika mchezo wake wa kwanza, hakuwa refa wa kati bali aliteuliwa kama mwamuzi wa akiba katika mechi ya Kombe la Shirikisho la Afrika kati ya Jaraaf ya Senegal na Platinum ya Zimbabwe, ambapo Jaraaf walishinda 1-0.

Licha ya kuwa na beji ya FIFA, safari ya Manet kuchezesha michezo ya klabu au timu za taifa barani Afrika bado inaonekana kuwa changa. Uzoefu wake kwenye uwanja wa kimataifa unahusisha mechi saba pekee, sita akiwa mwamuzi wa akiba na moja tu akiwa refa wa kati. Kwa hivyo, mtanange wa Simba SC dhidi ya Al Ahli utakuwa mchezo wake wa kwanza kama mwamuzi wa kati katika mechi ya klabu za Afrika.

Mtihani Mkubwa kwa Manet

Mchezo huu wa Jumapili ni muhimu si tu kwa timu hizo mbili, bali pia kwa Manet mwenyewe. Hii ni mara yake ya kwanza kuchezesha mechi kubwa ya klabu barani Afrika, huku macho ya mashabiki na wachambuzi yakimwangalia kwa karibu. Kutokuwa na uzoefu wa michezo mingi ya kimataifa kunampa changamoto ya kuthibitisha uwezo wake mbele ya timu mbili zenye mashindano makali.

Licha ya kutopata fursa nyingi za kuchezesha mechi kubwa, Manet alishiriki kwenye mechi ya kufuzu kwa AFCON kati ya Zimbabwe na Cameroon mnamo Septemba 10, 2023, ambayo ilimalizika kwa sare ya bila kufungana. Ingawa haikuwa mechi ya vilabu, huo ulikuwa mtihani wa kwanza kwake kama mwamuzi wa kati kwenye mechi ya timu za taifa.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Elie Mpanzu Kwenye Rada za Yanga na Simba
  2. Yanga Yafanya ‘Homework’ ya Kutosha, Gamondi Apania Tiketi ya Makundi
  3. Fadlu Davids Afurahishwa na Ngome ya Ulinzi Simba
  4. Zahera Aanza Tambo Baada ya Ushindi wa Kwanza wa Namungo Ligi Kuu
  5. Azam FC Yalenga Ushindi wa Kwanza Ligi Kuu Dhidi ya Simba
  6. Gamondi Apania Ushindi Mnono Mechi ya Marudiano Dhidi ya CBE
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo