Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024

Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024 | LATRA Yatangaza Nauli za SGR, Safari Kuanza Hivi Karibuni

Watanzania wanaosubiri kwa hamu uzinduzi wa safari za treni ya mwendokasi (Standard Gauge Railway – SGR) sasa wana sababu ya kutabasamu. Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imezindua rasmi nauli zitakazo tumika kwenye safari za treni ya mwendokasi kwa mwaka 2024, huku safari za abiria kutajwa kuanza hivi karibuni. Huu ni wakati wa kihistoria kwa sekta ya usafiri wa reli nchini, kwani SGR inatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa katika jinsi tunavyosafiri.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na LATRA, nauli za SGR zimewekwa kwa kuzingatia umbali wa safari na umri wa abiria, hivyo kuhakikisha kuwa usafiri huu wa kisasa unakuwa nafuu na haki kwa Watanzania wote. Kuanzia Dar es Salaam hadi Pugu, Morogoro, Dodoma, na hata mikoa ya mbali zaidi kama Makutupora, sasa unaweza kusafiri kwa treni ya kisasa, yenye kasi na urahisi usio na kifani.

Lakini kabla ya kuanza kwa safari hizi za zinazotegemea kua mkombozi mkubwa, LATRA imeweka masharti kadhaa muhimu ili kuhakikisha usalama na ufanisi wa huduma za SGR. Shirika la Reli Tanzania (TRC) linapaswa kutimiza masharti haya, ikiwa ni pamoja na kuwa na leseni ya usafirishaji, kuhakikisha miundombinu na mabehewa yapo salama, na kutumia mfumo wa kisasa wa utoaji tiketi za kielektroniki.

Huu ni mwanzo wa enzi mpya katika usafiri wa reli nchini Tanzania. SGR inakuja na ahadi ya safari za haraka, salama, na za kustarehesha, zikiunganisha miji na mikoa yetu kwa njia ya kisasa na ya kuaminika.

Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024

Muundo wa Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024

Nauli za SGR zimewekwa kwa kuzingatia umbali wa safari usika na umri wa abiria. Kwa watu wazima na watoto wenye umri zaidi ya miaka 12, nauli imetajwa kuwa ni Tsh. 69.51 kwa kila kilomita. Watoto wenye umri kati ya miaka 4 na 12 watalipa nusu ya bei hiyo, yaani Tsh. 34.76 kwa kilomita. Watoto chini ya miaka minne watasafiri bure, lakini taarifa zao zitahitajika kurekodiwa.

Hizi ndizo Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024 Kwa Abiria Wenye umri zaidi ya miaka 12

Mchanganuo wa nauli hizo kwa daraja la kawaida kulingana na umbali wa vituo kuanzia Dar es Salaam hadi Makutupora kwa watu wazima na watoto wenye umri zaidi ya miaka 12 ni kama ifuatavyo;

Safari   Umbali (Km) Nauli (Shilingi)
Kutoka Kwenda Daraja la Kawaida
Dar es Salaam Pugu 19 1000
Dar es Salaam Soga 51 4000
Dar es Salaam Ruvu 73 5000
Dar es Salaam Ngerengere 134.5 9000
Dar es Salaam Morogoro 192 13000
Dar es Salaam Mkata 229 16000
Dar es Salaam Kilosa 265 18000
Dar es Salaam Kidete 312 22000
Dar es Salaam Gulwe 354.7 25000
Dar es Salaam Igandu 387.5 27000
Dar es Salaam Dodoma 444 31000
Dar es Salaam Bahi 501.6 35000
Dar es Salaam Makutupora 531 37000

Nauli za Treni ya Mwendokasi SGR 2024 Kwa Abiria Wenye umri Kuanzaia Miaka 4 hadi 12

Aidha, mchanganuo wa nauli kwa daraja la kawaida kulingana na umbali wa vituo kuanzia Dar es Salaam hadi Makutupora kwa watoto wenye umri kuanzia miaka minne (4) hadi 12 ni kama ifuatavyo;

Safari Umbali (Km) Nauli (Shilingi)
Kutoka Kwenda Daraja la Kawaida
Dar es Salaam Pugu 19 500
Dar es Salaam Soga 51 2000
Dar es Salaam Ruvu 73 2500
Dar es Salaam Ngerengere 134.5 4500
Dar es Salaam Morogoro 192 6500
Dar es Salaam Mkata 229 8000
Dar es Salaam Kilosa 265 9000
Dar es Salaam Kidete 312 11000
Dar es Salaam Gulwe 354.7 12500
Dar es Salaam Igandu 387.5 13500
Dar es Salaam Dodoma 444 15500
Dar es Salaam Bahi 501.6 17500
Dar es Salaam Makutupora 531 18500

Masharti Kabla ya Safari Kuanza

LATRA imetoa masharti kadhaa ambayo yanapaswa kutimizwa kabla ya kuanza kwa safari za SGR. Masharti haya ni pamoja na:

  • Shirika la Reli Tanzania (TRC) kuwa na leseni ya usafirishaji
  • Miundombinu ya reli na mabehewa kuwa na ithibati ya usalama
  • Matumizi ya mfumo wa utoaji tiketi za kielektroniki
  • Kuunganishwa kwa mfumo wa tiketi na mifumo ya LATRA
  • Uwepo wa watumishi waliothibitishwa na waliosajiliwa na LATRA

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Nauli ya Basi Dar Es Salaam kwenda Morogoro 2024
  2. Bei Ya Friji Za Boss 2024 | Friji Za Boss Na Bei Zake
  3. Nauli ya Basi Dar Es Salaam kwenda Dodoma 2024
  4. Jinsi Ya Kupata Leseni Ya Biashara Ya Duka La Rejareja
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo