Matokeo Kagera Sugar vs JKT Tanzania Leo September 16 2024

Matokeo Kagera Sugar vs JKT Tanzania Leo September 16 2024 | Matokeo ya Kagera Sugar Leo vs JKT Tanzania

Kagera Sugar leo watawakalibisha JKT Tanzania katika mchezo wa ligi kuu ya NBC Tanzania 2024/2025 ambao utaanza kutimua vumbi katika uwanja wa Kaitaba Bukoba Kagera majira ya saa Moja kamili usiku. Mchezo huu ni muhimu sana kwa Kagera Sugar ambao wamekua na mwanzo mbuvu ambapo wameshindwa kupata hata pointi moja katika mechi tatu za ligi walizocheza.

Kagera Sugar, wakijulikana kwa jina la utani Wanankulukumbi, wameanza msimu huu wa 2024/2025 kwa matokeo ya kusikitisha. Katika michezo yao mitatu ya mwanzo, wamepoteza yote bila kujikusanyia pointi yoyote.

Timu hii inatoka kwenye matokeo mabaya, ikipoteza dhidi ya Singida Black Stars kwa 1-0, kufungwa na mabingwa watetezi Yanga SC kwa 2-0, na kisha kupokea kipigo kingine cha 1-0 kutoka kwa Tabora United.

Licha ya mwanzo mbovu, Kagera Sugar wanalazimika kuonyesha uthabiti leo ili kuepuka kuendelea kuporomoka kwenye msimamo wa ligi. Ushindi katika mechi hii unaweza kuwapa motisha kubwa ya kurudi kwenye njia sahihi. Kocha wa kagera sugar Paul Nkata bila shaka atakuwa na mbinu mpya ili kuvunja ukame wa pointi ambao umekuwa ukiwakumba.

Matokeo Kagera Sugar vs JKT Tanzania Leo September 16 2024

Kagera Sugar  VS JKT Tanzania

🏆 Tanzania NBC Premier League
Kagera Sugar Fc🆚 JKT Tanzania Fc
📆 16 September 2024
🏟️ Kaitaba Stadium
⏱️ 19:00
📺 Azam Tv

Matokeo Kagera Sugar vs JKT Tanzania Leo September 16 2024

Kikosi cha Kagerasugar Leo VS JKT Tanzania

  • 28 Chalamanda
  • 06 Chilo
  • 24 Mfuko
  • 11 Kapama
  • 04 Onditi [C]
  • 15 Manyasi
  • 46 Mahundi
  • 18 Athuman
  • 20 Lwasa
  • 40 Tariq
  • 50 Emmanuel

Wachezaji wa Ziada: Kipao, Salehe, Bukenya, Mussa, Andrew, Mwijage, Momo, Luhende, Datius, Mafie

JKT Tanzania: Kusaka Ushindi Baada ya Sare ya Kwanza

Kwa upande wa JKT Tanzania, timu hii inaingia katika mchezo wa leo ikiwa na alama moja tu baada ya kutoka sare ya 1-1 dhidi ya Azam FC katika mchezo wao wa kwanza wa msimu. Sare hiyo iliwaonyesha mashabiki wa JKT kuwa timu yao ina uwezo wa kupambana na timu kubwa za ligi, lakini sasa wanahitaji ushindi wa kwanza ili kujiweka kwenye nafasi nzuri katika msimamo wa ligi.

Kwa kumkabili Kagera Sugar leo, JKT Tanzania wana fursa nzuri ya kuongeza pointi tatu muhimu. Ushindi huu utawapa morali kubwa na kuwafanya wawe kwenye nafasi bora katika ligi.

Je, Mchezo Utakuwaje?

Mchezo wa leo unatarajiwa kuwa wa ushindani mkali. Kagera Sugar wanahitaji ushindi wa haraka ili kujiinua kutoka kwenye mkwamo wa matokeo mabaya, huku JKT Tanzania nao wakiwa na hamasa ya kuondoka na pointi zote tatu. Wachezaji wa Kagera Sugar kama vile mshambuliaji wao hatari Emmanuel, wanatarajiwa kutoa mchango mkubwa kwenye mchezo huu.

Kwa upande wa JKT Tanzania, safu yao ya ulinzi imeonekana kuwa imara kwenye mchezo wa kwanza, na leo watahitaji kuonyesha uimara huo tena ili kukabiliana na mashambulizi ya Wanankulukumbi. Pia, safu yao ya ushambuliaji inatakiwa kuwa makini sana ili kutumia nafasi chache wanazoweza kupata mbele ya goli.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Viingilio Mechi ya Simba Vs Al Ahli Tripoli 22/09/2024
  2. Ahmed Ally Athibitisha Usalama wa Kikosi cha Simba Libya
  3. Stephanie Aziz KI Sasa Aiwaza Mechi ya Zanzibar
  4. Gamondi Aonesha Kutoridhishwa na Ubora wa Washambuliaji
  5. Ratiba ya Mechi za Ligi Kuu ya NBC Leo 16 September 2024
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo