Mashujaa FC Yafunga Dirisha la Usajili kwa Kumnasa Kibaya

Mashujaa FC Yafunga Dirisha la Usajili kwa Kumnasa Kibaya

Katika dkika za mwisho kabisa za usajili mkuu kabla ya kuanza kwa msimu mpya, klabu ya Mashujaa FC imetangaza kumsajili kiungo mshambuliaji mwenye uwezo mkubwa, Jaffar Kibaya, akitokea Singida Black Stars. Usajili huu unaashiria nia ya dhati ya Mashujaa kuimarisha kikosi chao na kujiandaa vyema kwa changamoto za Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao.

Kibaya, anayejulikana kwa uwezo wake wa kushambulia na kutengeneza nafasi za mabao, anatarajiwa kuongeza makali kwenye safu ya ushambuliaji ya Mashujaa FC. Uamuzi wa kumsajili umetokana na benchi la ufundi la klabu hiyo kuvutiwa na kiwango chake cha uchezaji.

Baada ya kukamilisha usajili, jukumu sasa linabaki kwa Kocha Mkuu, Mohamed Abdallah ‘Bares’, kuunganisha wachezaji wapya na wa zamani ili kuunda timu yenye ushindani. Kikosi cha Mashujaa FC sasa kinaonekana kuwa na nguvu zaidi, na mashabiki wanatarajia kuona matokeo chanya uwanjani.

Mashujaa FC Yafunga Dirisha la Usajili kwa Kumnasa Kibaya

Uzoefu wa Kibaya

Kabla ya kujiunga na Singida Black Stars, Kibaya alikuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha Mtibwa Sugar kwa misimu kadhaa. Uzoefu wake katika Ligi Kuu unatarajiwa kuwa msaada mkubwa kwa Mashujaa FC, hasa katika msimu wao wa pili kwenye ligi kuu.

Mashabiki wa Mashujaa FC hawatasubiri kwa muda mrefu kumuona Kibaya akiwa kazini. Mchezaji huyo anatarajiwa kuanza kuitumikia klabu yake mpya Jumamosi ijayo, wakati Mashujaa FC itakapocheza dhidi ya Dodoma Jiji kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika.

Usajili wa Kibaya unafuatia usajili mwingine mkubwa uliofanywa na Mashujaa FC msimu huu, ikiwa ni pamoja na Seif Karihe kutoka Mtibwa Sugar, Chrispin Ngushi kutoka Yanga, Abdulmalik Zacharia kutoka Namungo, na wengine wengi.

Maandalizi ya Msimu Mpya Yanaendelea

Mashujaa FC imekuwa ikijiandaa kwa msimu mpya kwa kufanya mazoezi na mechi za kirafiki. Jumamosi iliyopita, walicheza dhidi ya Inter Star ya Burundi kwenye mechi ya Kilele cha Tamasha la Mashujaa Day na kuibuka na ushindi wa mabao 4-1.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Cv ya Leonel Ateba Mshambuliaji Mpya wa Simba 2024/2025
  2. “Nilipe Nisepe Zangu” – Ngoma Aamsha Dude Simba SC
  3. Viwanja Vitakavyo Tumika Mechi za Ligi Kuu 2024/2025
  4. Mzize Amtaja Chama Kuwa na Jicho la Pasi
  5. Liverpool Imechukua EPL Mara Ngapi
  6. Bingwa Wa Ngao ya Jamii 2024 ni Yanga Sc, Yailaza Azam FC 4-1 Katika Fainali
  7. Matokeo Yanga VS Azam Leo Fainali Ngao ya Jamii 2024
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo