Majina Ya Walimu Walioitwa Kwenye Usaili 2024

MAJINA ya Walioitwa kwenye Usaili Ajira za Walimu 2024 MDAs LGAs

Majina Ya Walimu Walioitwa Kwenye Usaili 2024 | Tangazo La Kuitwa kwenye Usaili Walimu

Kama wewe ni miongoni mwa maelfu ya waombaji wa nafasi za kazi ya ualimu zilizotangazwa na Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa (MDAs & LGAs) kupitia Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma mwezi Agosti 2024, basi habari njema ni kwamba majina ya walioitwa kwenye usaili yametangazwa rasmi.

Baada ya muda mrefu wa kusubiri kwa hamu, hatimaye orodha ya majina ya walimu waliofuzu hatua ya awali imetolewa, ikiwapa fursa ya kuendelea katika mchakato wa kuwania nafasi hizo muhimu katika sekta ya elimu nchini.

Tangazo hili la majina linaashiria hatua muhimu katika safari ya waombaji hawa kuelekea kutimiza ndoto zao za kuwa walimu. Ni wakati wa kujipanga vyema kwa ajili ya usaili, ambao utakuwa ni kipimo cha uwezo, ujuzi, na umahiri wao katika fani hii adhimu.

Katika makala haya, tutakufahamisha kwa undani kuhusu orodha ya majina ya walioitwa kwenye usaili, kada za ualimu zilizo na nafasi, maelekezo muhimu kwa ajili ya usaili, na ushauri kwa waombaji wote. Aidha, tutawaletea tahadhari muhimu zinazopaswa kuzingatiwa na waombaji ili kuepuka usumbufu wowote katika mchakato huu.

Orodha ya majina ya walimu walioitwa kwenye usaili inahusisha kada mbalimbali, ikiwemo:

  • Mwalimu Daraja la III A & B Elimu Maalum
  • Mwalimu Daraja la III B & C Somo la Biashara
  • Mwalimu Daraja la III B & C Kifaransa
  • Mwalimu Daraja la III B & C Kilimo
  • Mwalimu Daraja la III B & C Somo la Lishe
  • Mwalimu Daraja la III B & C Somo la Ushonaji
  • Fundi Sanifu Maabara ya Shule Daraja la II
  • Mwalimu Daraja la III B Fasihi ya Kiingereza
  • Mwalimu Daraja la III B Kiingereza
  • Mwalimu Daraja la III C Hisabati
  • Mwalimu Daraja la III C Fizikia
  • Mwalimu Daraja la III B Hisabati
  • Mwalimu Daraja la III B Fizikia
  • Mwalimu Daraja la III C Kemia, Shule ya Msingi, Elimu Maalumu, Uraia na Kilimo
  • Mwalimu Daraja la III C Baiolojia, Tehama na Uchumi
  • Mwalimu Daraja la III C Kiingereza na Fasihi ya Kiingereza
  • Mwalimu Daraja la III C Historia
  • Mwalimu Daraja la III C Jiografia
  • Mwalimu Daraja la III C Kiswahili
  • Mwalimu Daraja la III B
  • Mwalimu Daraja la IIIA

Majina Ya Walimu Walioitwa Kwenye Usaili 2024

Habari njema kwa waombaji wote wa nafasi za ualimu! Majina ya wale waliofuzu hatua ya awali na kuitwa kwenye usaili yametangazwa rasmi. Sasa unaweza kuangalia kama jina lako liko kwenye orodha kwa mujibu wa kada uliyoiomba.

Ili kurahisisha utafutaji wako, tumekuandalia viungo vya moja kwa moja vinavyokupeleka kwenye orodha ya majina kwa kila kada. Bofya kiungo cha nafasi ya kazi uliyoiomba ili kuona orodha na uhakikishe kama umechaguliwa kuendelea na hatua inayofuata ya usaili.

  1.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La III A & B Elimu Maalum, Mwalimu Daraja La III B & C Somo La Biashara 16-10-2024
  2.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Darala III B & C Kifaransa, Kilimo, Somo La Lishe, Somo La Biashara, Somo La Ushonaji Na Fundi Sanifu Maabara Ya Shule Daraja La Ii 16-10-2024
  3.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La III B Fasihi Ya Kiingereza 15-10-2024
  4.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La III B Kiingereza 15-10-2024
  5.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La III C Hisabati , Fizikia Na Mwalimu Daraja La III B Hisabati 15-10-2024
  6.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La III B Fizikia 15-10-2024
  7.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La III C Kemia, Shule Ya Msingi, Elimu Maalumu, Uraia Na Kilimo 15-10-2024
  8.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La III C Baiolojia, Tehama Na Uchumi 15-10-2024
  9.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La III C Kiingereza Na Fasihi Ya Kiingereza 15-10-2024
  10.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La III C Historia 15-10-2024
  11.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La III C Jiografia 15-10-2024
  12.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La III C Kiswahili 15-10-2024
  13.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La III B 15-10-2024
  14.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja IIIb 15-10-2024
  15.  Tangazo La Kuitwa Kwenye Usaili Mwalimu Daraja La IIIa 15-10-2024

Majina Ya Walimu Walioitwa Kwenye Usaili 2024

Maelezo Muhimu Kuhusu Usaili

Kwa waombaji walioitwa kwenye usaili, kuna mambo muhimu ya kuzingatia kabla ya kufika kwenye eneo la usaili. Mchakato wa usaili unategemea taratibu zilizowekwa na serikali ili kuhakikisha usaili unafanyika kwa ufanisi na kwa mujibu wa kanuni zilizopo.

Haya ni baadhi ya maelekezo muhimu kwa waombaji wote walioweza kuona majina yao kwenye orodha ya walioittwa kwenye usaili:

  1. Usaili utafanyika kuanzia tarehe kama ilivyooneshwa kwenye tangazo hili muda na sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila Kada.
  2. Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa Barakoa (Mask)
  3. Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi;
  4. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho cha Mpiga kura,Kitambulisho cha kazi,Kitambulisho cha Uraia, Hati ya kusafiria, Leseni ya Udereva au barua  ya utambulisho kutoka Serikali ya Mtaa/Kijiji unachotoka.
  5. Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha kuzaliwa,kidato cha IV,
  6. VI, Astashahada, Stashahada,Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na sifa za Mwombaji.
  7. Wasailiwa watakaowasilisha Testimonials, Provisional Results, Statement of results, hatiza matokeo za kidato cha IV na VI (form V and form VI results slips) HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI.
  8. Kila msailiwa atajigharamia kwa Chakula, Usafiri na Malazi.
  9. Kila Msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili.
  10. Kwa waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe Vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (kama TCU, NACTE au NECTA)
  11. Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa hawakukidhi Hivyo, wasisite kuomba tena pindi nafasi za kazi zitakapotangazwa na kuzingatia mahitaji  ya tangazo husika.
  12. Kwa kada ambazo wanatakiwa kusajiliwa na Bodi zao za Kitaaluma wanapaswa kuja na vyeti vyao Halisi vya Usajili pamoja na Leseni za kufanyia kazi.
  13. Wasailiwa wote walioitwa kwenye usaili wahakikishe wanaingia kwenye akaunti zao na kunakili namba ya mtihani kwa kuwa namba hizo hazitatolewa iku ya usaili

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Majina ya Walioitwa kwenye Usaili Ajira za Walimu 2024 MDAs & LGAs
  2. Majina ya Walioitwa kwenye Usaili Ajira Portal 2024
  3. Nafasi 4 za Kazi ya Dereva Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa | Mwisho 27 Oktoba 2024
  4. Nafasi za Kujiunga na JKT 2024/2025
  5. Majina ya Walioitwa Kwenye Usaili NECTA Oktoba 2024
  6. Sifa za Kujiunga na JKT 2024, Mafunzo ya Kujitolea
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo