Kocha wa Simba SC, Fadlu Davids atangazwa Kocha Bora wa mwezi Agosti

Kocha wa Simba SC, Fadlu Davids atangazwa Kocha Bora wa mwezi Agosti

Simba SC imeendelea kudhihirisha uwezo wake wa kusaka mafanikio kwenye Ligi Kuu ya NBC baada ya kocha wao mkuu, Fadlu Davids, kutangazwa Kocha Bora wa Mwezi Agosti. Tuzo hii ni matokeo ya mafanikio makubwa aliyoyapata kocha Davids katika kuiongoza Simba SC kwenye mechi zake mbili za kwanza za ligi, ambapo timu yake iliibuka na ushindi wa mabao 7 bila ya kufungwa.

Fadlu Davids amewapiku makocha wenzake, Patrick Aussems wa Singida Black Stars na Mohamed Abdallah wa Mashujaa, ambao walikuwa naye kwenye kinyang’anyiro cha tuzo ya kocha bora wa mwezi Agosti.

Fadlu Davids, raia wa Afrika Kusini mwenye umri wa miaka 43, alijiunga na Simba SC Julai 5, 2023, akichukua nafasi ya Abdelhak Benchikha. Katika kipindi kifupi tangu alipowasili, tayari ameweka alama yake ndani ya klabu hii kubwa ya Tanzania, na kuwa miongoni mwa makocha waliowahi kuanza vizuri msimu mpya wa ligi ndani ya misimu 10 iliyopita.

Kocha wa Simba SC, Fadlu Davids, atangazwa Kocha Bora wa mwezi Agosti

Katika mwezi wa Agosti, Davids aliwaongoza Simba SC kwenye mechi mbili za ligi dhidi ya Tabora United na Fountain Gate, na kushinda zote kwa matokeo ya 3-0 na 4-0 mtawalia. Ushindi huu wa mabao saba bila majibu umeonyesha mbinu na uwezo wa kocha huyu mpya, ambaye analenga kuifanya Simba kuwa timu imara zaidi katika michuano ya ndani na kimataifa.

Kipindi cha dakika 180 ambazo Davids amekuwa akiiongoza Simba SC, kimekuwa na mafanikio makubwa kwa timu hiyo, na kwa kiasi kikubwa ameweza kujidhihirisha kama kocha mwenye uwezo wa kuleta matokeo mazuri.

Rekodi yake ya mabao saba bila kufungwa katika mechi mbili za kwanza ni alama ya matumaini kwa mashabiki wa Simba SC, ambao wanaendelea kumuunga mkono kocha wao mpya katika safari hii ya msimu wa 2023/2024.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Ratiba ya Timu ya Taifa Wasichana U17 (Serengeti Girls) UNAF Tunisia 2024
  2. Ratiba YA Ligi Kuu Ya Zanzibar (Pbz Premier League) 2024/2025
  3. Vilabu Bora Afrika 2024/2025 (CAF Club Ranking)
  4. Kikosi cha Taifa Stars Kufuzu AFCON 2025
  5. Mbeya City Day Rasmi Kufanyika Septemba 7
  6. Yanga, Simba, Azam FC Watoa Wito kwa Mashabiki Kuelekea AFCON
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo