Kikosi cha Azam Fc VS APR Leo 24/08/2024

Kikosi cha Azam Fc VS APR Leo 24/08/2024 | Kikosi cha Azam Leo Dhidi ya APR Klabu Bingwa CAF

Wana rambaramba Azam Fc leo watakua ugenini Rwanda kuikabili APR Fc katika mchezo wa marudiano wa hatua za awali za michuano ya klabu bingwa Afrika (CAF champions league). Mchezo huu utaanza majira ya saa moja usiku katika uwanja wa Amahoro, Kigali. Azam Fc itaingia uwanjani ikiwa na faida ya ushindi wa bao 1-0 walioupata katika mchezo wa kwanza uliopigwa jijini Dar es salaam wiki iliyopita.

Azam FC imesafiri na msafara mkubwa wa watu 60, wakiwemo wachezaji, benchi la ufundi, na hata mashabiki wachache walioandamana nao ili kuongeza morali ya timu. Wachezaji wote waliokuwepo katika mchezo wa kwanza watakuwepo pia katika mchezo huu, wakiwa wamethibitishwa kuwa fiti kwa mtanange huu mgumu.

Kocha wa Azam FC, Youssoyuf Dabo, ameweka wazi kuwa lengo lao ni kulinda ushindi walioupata nyumbani, lakini pia wanataka kuongeza bao la mapema ili kuwafanya wenyeji APR wawe na kazi ngumu zaidi. Dabo anaamini kuwa wachezaji wake wana uwezo wa kupata ushindi hata ugenini, na wanataka kutumia nafasi watakazopata vizuri zaidi kuliko walivyofanya katika mchezo wa kwanza.

APR, mabingwa wa Rwanda, watakuwa na presha kubwa ya kusaka ushindi mnono ili kusonga mbele katika michuano hii. Wanatarajiwa kuja kwa kasi kubwa wakitumia faida ya kucheza nyumbani mbele ya mashabiki wao. Hata hivyo, Azam FC inajua ugumu wa mchezo huu na imejiandaa kukabiliana na mashambulizi ya wenyeji wao.

Kikosi cha Azam Fc VS APR Leo 24/08/2024

Kikosi cha Azam Fc VS APR Leo 24/08/2024

Kikosi cha Azam Fc kitakachoanza leo katika mchezo huu muhimu dhidi ya APR Fc kinatarajiwa kutangazwa rasmi majira ya saa 12 jioni. Endelea kufuatilia ukurasa huu, ambapo tutakuletea orodha kamili ya wachezaji 11 watakaopata nafasi ya kuitumikia timu yao katika mtanange huu mkali wa marudiano, kama watakavyotajwa na kocha mkuu wa Azam FC.

Kikosi cha Azam Fc VS APR Leo 24/08/2024

Mchezo huu unatarajiwa kuwa wenye ushindani mkubwa. Azam FC itacheza kwa nidhamu kubwa huku ikisaka bao la mapema ili kujiweka katika nafasi nzuri zaidi. APR nao watashambulia kwa nguvu zote ili kusawazisha bao la nyumbani na hatimaye kupata ushindi.

Mashabiki wa soka barani Afrika wanasubiri kwa hamu kuona ni nani atakayetoka kifua mbele katika mchezo huu wa marudiano.

Je, Azam FC itaweza kulinda ushindi wao na kusonga mbele, au APR watafanikiwa kupindua meza na kujihakikishia nafasi katika hatua inayofuata? Muda ndio utakaoamua.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Matokeo ya Yanga Vs Vitalo Leo 24/08/2024
  2. Kikosi cha Yanga Vs Vitalo Leo 24/08/2024
  3. Msimamo NBC Premier league 2024/2025 | Ligi Kuu Bara
  4. Usajili wa Chelsea 2024/2025
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo