Benchi Jipya La Ufundi Simba 2024/2025

Benchi Jipya La Ufundi Simba 2024/2025

Klabu ya Simba SC imejizatiti kwa kufanya mabadiliko makubwa katika benchi lake la ufundi kuelekea msimu wa 2024/2025. Mabadiliko haya yamepokelewa kwa furaha na mashabiki wengi wa wekundu wa Msimbazi, wakiamini kuwa yataimarisha kikosi na kuongeza matumaini ya kufanya vizuri katika michuano mbalimbali.

Kuondoka kwa Abdelhak Benchikha

Simba SC ilithibitisha kuondoka kwa kocha wake mkuu, Abdelhak Benchikha, kutokana na matatizo ya kifamilia. Kuondoka kwa Benchikha kulisababisha klabu kumaliza msimu uliopita chini ya kocha wa mpito, Juma Mgunda. Hata hivyo, uongozi wa Simba haukusita katika kutafuta mbadala mzuri na kuhakikisha kikosi kinaendelea kuwa na uimara.

Kocha Mpya na Benchi Lake

Simba SC hatimaye imemtangaza rasmi kocha mpya kwa msimu wa 2024/2025. Kocha huyu mpya amekuja na wataalamu mbalimbali ambao wataunda benchi la ufundi lenye uzoefu na weledi wa hali ya juu. Benchi Jipya La Ufundi Simba 2024/2025 linajumuisha:

Nafasi Jina Taifa
Kocha Msaidizi Darian Wilken Afrika Kusini
Kocha wa Makipa Wayne Sandilands Afrika Kusini
Kocha wa Viungo Riedoh Berdien Afrika Kusini
Mchambuzi Mueez Kajee Afrika Kusini

Benchi Jipya La Ufundi Simba 2024/2025

  1. Kocha Msaidizi – Atafanya kazi kwa karibu na kocha mkuu kuhakikisha mipango ya mazoezi na mbinu za mchezo zinatekelezwa kwa ufanisi.
  2. Kocha wa Makipa – Atahakikisha magolikipa wanapata mafunzo bora na kuwa katika hali nzuri ya kiakili na kimwili kwa ajili ya mechi zote.
  3. Kocha wa Viungo – Atahusika na mazoezi ya viungo, kuhakikisha wachezaji wanakuwa na nguvu, kasi, na stamina inayohitajika.
  4. Mchambuzi – Atachambua michezo, wachezaji, na wapinzani kwa kina ili kutoa taarifa muhimu zitakazosaidia kuandaa mikakati ya ushindi.

Matumaini na Malengo ya Simba SC

Lengo kuu la mabadiliko haya ni kuhakikisha Simba SC inakuwa na kikosi bora na chenye ushindani wa hali ya juu katika msimu wa 2024/2025. Uongozi wa klabu una matumaini makubwa kuwa benchi hili jipya la ufundi litasaidia klabu kufikia malengo yake, ikiwa ni pamoja na kutwaa mataji ya ligi kuu na michuano mingine ya kitaifa na kimataifa.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Hii apa CV ya Omary Abdallah Kiungo Mpya Wa Simba 2024/2025
  2. CV ya Fadlu Davids: Kocha Mpya wa Simba SC (2024/2025)
  3. Cv ya Valentino Mashaka Mshambuliaji Mpya wa Simba Sc 2024
  4. Picha za Wachezaji Wapya wa Simba 2024/2025
  5. Majina ya Wachezaji Wapya Simba 2024/2025
  6. CV Ya Abdulrazak Hamza Beki Mpya Wa Simba 2024/2025
  7. Wachezaji Waliosajiliwa Simba 2024/2025
  8. Tetesi za Usajili simba 2024/2025
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo