Muda wa Kutuma Maombi Nafasi za Kazi Jeshi la Polisi Waongezwa

Muda wa Kutuma Maombi Nafasi za Kazi Jeshi la Polisi Waongezwa; Serikali ya Tanzania yarefusha muda wa kutuma maombi ya kazi Jeshi la Polisi hadi Mei 21, 2024.

Je, wewe ni miongoni mwa maelfu ya vijana walioshindwa kutuma maombi ya kazi kwa nafasi zilizotangazwa na jeshi la poili kisa kukosa mtandao? Habari njema! Muda wa kutuma maombi ya nafasi za kazi zilizotangazwa na Jeshi la Polisi umeongezwa kwa siku tano zaidi, hadi tarehe 21 Mei 2024. Hii ni fursa ya dhahabu kwa vijana wote wenye sifa na nia ya kuitumikia Tanzania katika jeshi la la polisi.

Muda wa Kutuma Maombi Nafasi za Kazi Jeshi la Polisi Waongezwa

Habari njema kwa vijana wanaotamani kuvaa sare za Jeshi la Polisi, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetangaza rasmi kuongeza muda wa kutuma maombi ya nafasi mbalimbali za kazi. Awali, tarehe ya mwisho ilikuwa Mei 16, 2024, lakini kutokana na changamoto za kiufundi katika mtandao wa intaneti, muda huo umeongezwa kwa siku tano zaidi, hadi kufikia Mei 21, 2024.

Muda wa Kutuma Maombi Nafasi za Kazi Jeshi la Polisi Waongezwa

Habari hii ya kufurahisha imetolewa bungeni na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Hamad Masauni, baada ya Mbunge wa Makete, Festo Sanga, kuwasilisha hoja ya dharura kuhusu tatizo la intaneti lililoathiri vijana wengi waliotaka kutuma maombi yao. Serikali, kwa kuzingatia umuhimu wa kutoa fursa sawa kwa wote, imechukua hatua hii ya busara ili kuhakikisha kuwa hakuna kijana mwenye sifa atakayekosa nafasi ya kutimiza ndoto yake ya kujiunga na jeshi la polisi.

Fursa hii ya kipekee imefunguliwa kwa vijana wenye elimu ya kidato cha nne, kidato cha sita, astashahada, stashahada na shahada. Nafasi mbalimbali za kazi zinapatikana katika fani mbalimbali, ikiwemo uuguzi, famasia, uhandisi wa vyombo vya majini, kompyuta, muziki, upimaji ardhi, usimamizi wa michezo na utawala. Hii ina maana kwamba vijana wenye vipaji na ujuzi katika nyanja tofauti wanaweza kupata nafasi ya kutumia uwezo wao kutumikia nchi yao kupitia Jeshi la Polisi.

Ili kuhakikisha kuwa vijana wote wanaopenda kujiunga na Jeshi la Polisi wanapata taarifa hii muhimu, Serikali imeahidi kuendelea kufuatilia kwa karibu hali ya mtandao na kuchukua hatua zaidi ikiwa changamoto zitaendelea.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye, ametoa hakikisho kwamba juhudi za kurejesha mtandao katika hali yake ya kawaida zinaendelea kwa kasi, na hadi sasa asilimia 80 ya matengenezo imekamilika.

Vijana wenye sifa na nia ya kujiunga na Jeshi la Polisi wanashauriwa kutumia fursa hii ya ziada kutuma maombi yao kupitia tovuti rasmi ya ajira ya Jeshi la Polisi: ajira.tpf.go.tz. Maombi yote yanapaswa kuwasilishwa kabla ya tarehe ya mwisho, Mei 21, 2024, na waombaji wanapaswa kufuata maelekezo yote yaliyotolewa katika tangazo la awali la Mei 9, 2024.

Kama bado hujatuma maombi na una sifa zinazohitajika, usisite! Fursa bado ipo. Tembelea tovuti rasmi ya ajira ya Jeshi la Polisi, https://ajira.tpf.go.tz, na uwasilishe maombi yako kabla ya tarehe ya mwisho, Mei 21, 2024.

Mapendekezo Ya Mhariri: Nafasi Mpya Za Kazi Chuo Kikuu cha SUA: Mwisho wa Kutuma Maombi ni 19 Mei 2024

Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo