Code Za Mitandao Ya Simu Tanzania | Namba Za Simu Tanzania 2024

Code Za Mitandao Ya Simu Tanzania | Namba Za Simu Tanzania: Katika ulimwengu wa leo, simu za mkononi zimekuwa sehemu muhimu sana ya maisha ya kila siku. Kupitia simu hizi, watu wanaweza kuwasiliana kwa urahisi, kupata habari, na hata kufanya shughuli za kifedha wakati na mahali popote. Hata hivyo, nyuma ya utendaji wa simu hizi, kuna mfumo mkubwa ambao huwezesha mawasiliano haya kufanyika. Mojawapo ya mambo muhimu sana katika mfumo huu ni “Code za Mitandao ya Simu.”

Code za mitandao ya simu ni nambari zinazotumika kutambua na kutofautisha mitandao mbalimbali ya simu. Tanzania, kama nchi nyingine, ina mfumo wake wa code za mitandao ya simu ambazo hutumiwa na makampuni mbalimbali ya simu kote nchini. Kuelewa jinsi code hizi zinavyofanya kazi na kutrambua ni code gani inawakilisha nambari ya kampuni gani ni muhimu sana.

Hapa, tutachunguza kwa kina zaidi kuhusu code za mitandao ya simu Tanzania. Tutakupa mwanga juu ya jinsi ya kutambua code za mitandao ya simu mbalimbali, huku tukikusaidia kuwezesha ufahamu wako wa nambari hizi mpya kwa urahisi na haraka.

Muonekano Wa Namba Za Simu Tanzania

Nambari za simu zinazotumika nchini Tanzania zinaundwa na tarakimu 12, zinazojumuisha msimbo (Code) wa nchi (+255), msimbo wa mtandao (tarakimu 3), na nambari ya kipekee ya mteja (tarakimu 7).

Ili kumpigia simu mtu aliye Tanzania kutoka nje ya nchi, ni muhimu kufuata muundo huu:

  • Msimbo wa Nchi (+255): Huu ni msimbo wa kimataifa wa Tanzania, unaoashiria kuwa unapiga simu kwenda Tanzania.
  • Msimbo wa Mtandao (tarakimu 3): Huu hutambulisha kampuni ya simu ambayo mtu unayempigia anatumia. Kila kampuni ina misimbo yake maalum (kwa mfano, Vodacom: 075, Tigo: 065, Airtel: 078).
  • Nambari ya Mteja (tarakimu 7): Hii ni nambari ya kipekee inayomtambulisha mtu unayempigia ndani ya mtandao wake.

Mfano:

Ukimpigia mtu ambaye anatumia Vodacom Tanzania na namba yake ya mteja ni 1234567, utapiga: +255 75 1234567.

Mikoa Na Code Zake Za Simu

Mkoa Nambari
Dar es Salaam 22
Pwani, Kibaha, Kisarawe, Lindi, Morogoro, Mtwara 23
Zanzibar (Unguja & Pemba, pamoja na Chake Chake, Mkoani, Wete) 24
Mbeya, Rukwa, Ruvuma 25
Dodoma, Iringa, Nzega, Singida, Tabora 26
Arusha; Kilimanjaro, Moshi, Tanga 27
Bukoba, Kagera, Kigoma, Mara, Mwanza, Shinyanga 28

Code Za Mitandao Ya Simu Tanzania | Namba Za Simu Tanzania

Code Za Mitandao Ya Simu Tanzania | Namba Za Simu Tanzania

Nchini Tanzania, kila kampuni ya simu ina Code maalum ambayo inaitambulisha kampuni hiyo kwa watumiaji wake. Code hio wa mtandao, inaojulikana pia kama “Network Code” au “Mobile Network Code” (MNC), ni sehemu ya namba ya simu ya mteja inayomtambulisha mteja huyo kuwa anatumia mtandao wa kampuni fulani. Kwa mfano, namba ya simu ya Tanzania inaanza na code ya nchi ambao ni +255, ikifuatiwa na cade ya mtandao, na kisha namba ya kipekee ya mteja. Code ya mtandao hutofautiana kulingana na kampuni ya simu.

Code Za Mtandano wa Vodacom Tanzania

  • Code ya Mitandao (MNC): 0746, 0745, 0754, 0755

Code Za Mtandano wa Tigo Tanzania

  • Code ya Mitandao (MNC): 0712, 0713, 0714, 0715, 0716, 0652

Code Za Mtandano wa Airtel Tanzania

  • Code ya Mitandao (MNC): 0784, 0785, 0786, 0787, 0788, 0688

Code Za Mtandano wa Halotel Tanzania

  • Code ya Mitandao (MNC): 0768, 0769, 0620

Code Za Mtandano wa Zantel

  • Code ya Mitandao (MNC): 077

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Jinsi Ya Kuangalia Namba Ya Simu Airtel, Vodacom, TTCL, Tigo & Halotel
  2. Menu ya Kukopa Salio Halotel & Jinsi ya Kukopa Muda wa Maongezi
  3. Hizi Apa Code za Haloteli: Namba Muhimu Za Haloteli 2024
  4. Jinsi ya Kukopa Salio Airtel (Menu Ya Kukopa Salio Airtel)
  5. Jinsi ya Kukopa Salio Tigo (Menu Ya Kukopa Salio Tigo) 2024
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo