Azam FC Yasaini Mkataba wa Ushirikiano na Klabu ya Uswidi

Azam FC Yasaini Mkataba wa Ushirikiano na Klabu ya Uswidi

Katika hatua kubwa ya kuimarisha soka la vijana na kufungua milango ya fursa za kimataifa, klabu ya Azam FC imesaini mkataba wa ushirikiano wa miaka mitano na klabu ya AIK Football ya Sweden. Mkataba huu wa kihistoria unalenga kukuza vipaji vya wachezaji chipukizi wa Azam FC kupitia mafunzo na maendeleo katika kituo cha kukuza vipaji cha AIK Football.

Kupitia mkataba huu, wachezaji wenye vipaji vya hali ya juu kutoka kituo cha kukuza vipaji cha Azam FC watapata fursa ya kipekee ya kwenda Stockholm, Sweden, na kufanya mazoezi na timu ya vijana ya AIK Football. Wakiwa huko, watapata mafunzo kutoka kwa makocha na wataalamu wa kimataifa, na wale watakaoonyesha uwezo wa kipekee watapata nafasi ya kujiunga na kikosi cha kwanza cha AIK Football.

Makamu Mwenyekiti wa Azam FC, Omary Kuwe, ameelezea furaha yake kuhusu ushirikiano huu, akisema kuwa unatoa nafasi kwa wachezaji chipukizi wa Azam FC kutimiza ndoto zao za kucheza soka Ulaya. “Tunaamini kuwa ushirikiano huu utakuwa chachu ya maendeleo ya soka nchini Tanzania na kuzalisha wachezaji wenye uwezo wa kushindana kimataifa,” alisema Bw. Kuwe.

Azam FC Yasaini Mkataba wa Ushirikiano na Klabu ya Uswidi

AIK Football Yatafuta Vipaji Afrika

Ofisa Mtendaji Mkuu wa AIK Football, Fredrik Soderberg, ameonyesha kuridhishwa kwake na ushirikiano huu, akisema kuwa unawapa fursa ya kupata vipaji vipya kutoka Azam FC na Tanzania kwa ujumla. “Tunaamini kuwa Afrika ina hazina kubwa ya vipaji vya soka, na ushirikiano huu utatusaidia kuvigundua na kuviendeleza,” alisema Bw. Soderberg.

Mkataba wa Manufaa kwa pande Zote Mbili

Mkataba huu wa ushirikiano unatarajiwa kuleta manufaa kwa pande zote mbili. Azam FC itapata fursa ya kuendeleza wachezaji wake chipukizi katika mazingira ya kimataifa, wakati AIK Football itapata fursa ya kupata vipaji vipya kutoka Tanzania. Ushirikiano huu pia unatarajiwa kuchangia katika maendeleo ya soka nchini Tanzania kwa ujumla.

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Wydad Bado Katika Harakati za Kumsajili Mzize
  2. Kikosi cha Chelsea UEFA Conference League 2024/2025
  3. Bellingham Afuata Nyayo za Ronaldo, Aingia YouTube Rasmi
  4. Manchester United Yatangaza Kikosi cha Wachezaji 25 kwa Ajili ya Europa 2024-25
  5. Ufaransa Yashushiwa Kipigo cha Goli 3-1 na Itali
Nina uzoefu wa miaka zaidi 6 katika uandishi wa habari nchini Tanzania. Shauku yangu ni kuleta habari muhimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Michezo